Skip to main content

WADAU WA KUPINGA UDHALILISHAJI PEMBA WANG'AKA



 

NA HANIFA SALIM, PEMBA


WADAU wa kupinga udhalilishaji Kisiwani Pemba wamesema, kukimbizwa kwa watuhumiwa hususani kesi za wanafamilia na kesi ikawa ndio mwisho wake huku jamii ikilalamika kwamba askari wanachangia kuchelewa kufuatilia ni miongoni mwa changamoto walizokumbana nazo wakati wa utendaji wa kazi zao.

Waliyasema hayo katika kikao kazi cha kuwasiliasha ripoti kwa kipindi cha mwezi Januari hadi Juni mwaka huu kwa kamati za kupinga udhalilishaji Kisiwani humo, kilichofanyika ukumbi wa ofisi ya Chama cha waandishi wa habari wanawake (TAMWA) Mkanjuni Chake chake.

Afisa ustawi wa Wilaya ya Wete Salma Saleh Hamad, akiwasilisha ripoti ya udhalilishaji wa wanawake na watoto kwa kipindi cha miezi sita, alisema kuchelewa kwa kipimo cha DNA na rushwa muhali bado pia ni changamoto kubwa kwa jamii. 

Alisema, malalamiko 64 ya matunzo na mvutano wa malezi yaliripotiwa katika kitengo cha ustawi wa jamii, ikiwemo 39 ya matunzi ya watoto na 25 ni mvutano wa malezi, ambapo malalamiko hayo yalipatiwa ufumbuzi na mawili yanaendelea kusikiliza katika ofisi zao za Wilaya.

Akichangia mada katika mkutano huo Makame Kombo Makame kutoka Mahakama ya Mkoa Wete alisema, ili ndoa ziweze kusimama zinahitaji msingi na msingi huo ni wazazi na ofisi ya kaadhi kutoa elimu ya ndoa kwa wanandoa kabla ya kufunga ndoa ili kuepuka udhalilishaji kwa watoto.

Ishaka Sultani Said kutoka TUJIPE alisema, katika utendaji wa kazi zao walibaini kwamba uwelewa mdogo kwa masuala ya udhalilishaji kwa jamii ya Wilaya ya Micheweni ni mdogo hivyo elimu inahitajika kwao.

"Jamii bado haijakubali kujitoa katika kuondosha udhalilishaji licha ya viongozi wa Wilaya na Mkoa wa Kaskazini kuwa tayari kupambana kwenye masuala haya lakini bado jamii haijawa na uthubutu", alisema.

Mwendesha mashitaka kutoka ofisi ya Mkurugenzi wa mashitaka DPP Mussa Khamis akiwasilisha ripoti ya ofisi hiyo Mkoa wa Kusini alisema, wamepokea majalada ya kesi za udhalilishaji 66 ambapo kati ya hayo 37 yalifunguliwa mahakamani.

Nae Abdalla Issa Abdalla kutoka chuo cha mafunzo Pemba alisema, kuanzia mwezi Januari hadi Juni wamepokea wanafunzi sita, huku wakiwa na watuhumiwa 37 ambao bado mashauri yao yanaendelea na upelekezi.

Mapema, akifungua mkutano huo kwa niaba ya Katibu tawala Wilaya ya Mkoani Muumini Abeid alisema, uwepo wa kamati hizo unalenga dhana ya kulinusuru taifa kwani, udhalilishaji ni janga ambalo lipo na linaendelea kuitia dosari nchi yao.

"Mashirikiano ni jambo muhimu katika kutokomeza janga hili la udhalilishaji wa wanawake na watoto, lazima jamii tuwe tayari kila mmoja kwa nafasi yake aoneshe utayari wa kupambana na hili naamini hapo tutafanikiwa kupunguza matendo haya", alisema.

Kwa upande wake Mratibu wa Tamwa Pemba Fat-hiya Mussa Said alisema, wadau hao kazi yao kubwa ni kutoa elimu kwa jamii kuhusiana na masuala mbali mbali ya udhalilishaji, kuibua kesi katika jamii pamoja na kutoa msaada wa kisheria na kisaikolojia kwa hatua za mwanzo wakati yanapotokea matukio ya udhalilishaji.

"Tunawasaidia wahanga wanapotokewa na matukio ili waweze kuziripoti kesi na kuwapa moyo wakati wanapofanya ufuatiliaji wa kesi hizo kwa kwenda nao mahakamani, kituo cha mkono kwa mkono na wanapovunjika moyo sisi tunakwenda kuwatia ari, ili kwa pamoja haya mapambano yaweze kufanikiwa", alisema.

Hata hivyo alisema, watuhumiwa wengi ambao wanaripotiwa na kesi za udhalilishaji hutoroka hivyo, alivishauri vyombo vya sheria kuhakikisha wanawarudisha watuhumiwa pamoja na kuwadhibiti ili wasikimbie baada ya kufanya kosa.
                        
                             MWISHO.

Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch