Skip to main content

Posts

WANANCHI WASHAURIWA KUPELEKA KERO ZAO KWA WASAIDIZI WA SHERIA

  IMEANDIKWA NA FATMA HAMAD, PEMBA@@@@ WANANCHI wametakiwa kuwatumia wasaidizi wa Sheria waliomo shehiani mwao, ili kupatiwa msaada wa kisheria kwalengo la kupata haki zao za msingi. Kauli hiyo ilitolewa na Afisa Sheria kutoka Ofisi ya Rais Katiba Sheria na Utawala bora Zanzibar Salma Suleiman wakati akizungumza na wananchi na wanafunzi wa Skuli ya Sekondari Msuka, katika mkutano maalumu wa kuijengea uwelewa jamii juu ya masuala ya kisheria, uliofanyika Skuli ya Sekondari Msuka wilaya yaMicheweni Kaskazini Pemba. Alisema Wananchi waliowengi wamekua wakipata matatizo mbali mbali ikiwemo migogoro ya ndoa, Ardhi pamoja na utelekezwaji, lakini bado uwelewa wa kuwatumia wasaidizi wa Sheria katika kuzitatua changamoto hiyo. Alisema kazi kubwa ya Wasaidizi wa Sheria ni kuhakikisha wanatoa msaada wa kisheria katika Jamii, hivyo ni mihimu kwa jamii kuwatumia wasaidizi hao, ili kupata ufumbuzi wa changamoto. ‘’Wasaidizi wa Sheria ni watu ambao wanatambulika kisheria, hivyo watumien...

MAMA MARIAM MWINYI: 'WAZAZI ZINGATIENI MALEZI NA MAKUZI BORA KWA WATOTO'

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA  MKE wa Rais wa Zanzibar, Msarifu na Mwenyekiti wa Bodi ya Wadhamini wa Taasisi ya Zanzibar Maisha Bora Foundation (ZMBF), Mama Mariam Mwinyi amesema ana imani kuwa malezi na makuzi bora ya awali ya mtoto ni msingi imara wa kujenga taifa lenye raia wenye afya, elimu, nidhamu na maendeleo endelevu. Mama Mariam Mwinyi ameyasema hayo Agosti 13, mwaka 2025, wakati alipozindua Kampeni ya Malezi na Makuzi ya Awali ya Mtoto wa Zanzibar (ECD) katika viwanja vya Kisonge, Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja. Amesema kuwa, ni vyema kwa jamii kuhakikisha inawapatia watoto malezi na makuzi bora ya awali, ili kuwajengea mustkbali wa maisha bora ya baadae. Mama Mariam Mwinyi ameeleza kuwa, ZMBF imekuwa mstari wa mbele kusaidia maendeleo ya makuzi ya mtoto, hususan katika programu za lishe pamoja na huduma za afya ya mama na mtoto, ambapo kupitia jitihada hizo, imeweza kuwafikia wanufaika zaidi ya 50,000 katika Shehia 67 na vijiji 644 vya Unguja na Pemba. Al...

UZINDUZI WA PROGRAMU YA ECD ZANZIBAR: UTPC yawanoa waandishi wa habari visiwani, 'Jamii yatakiwa kuzingatia malezi na makuzi bora kwa watoto wao'

                 IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@    KILA tuamkapo asubuhi, wazazi wengi wana tabia ya kukimbilia sehemu zao za kazi kuliko kumkimbilia mtoto wake aliepo nyumbani.   Lakini hii ni kwa sababu watoto huchelewa kuamka ndipo mama huona ni bora kumuacha amalize usingizi wake, huku akijua hatoonana nae kwa masaa tisa baadae.   Inasikitisha sana kuona kwamba wazazi wa zama hizi hawana muda wa kuwashughulikia watoto, hawachezi nao na wala hawawajengei mazingira bora ya kumfanya achangamke kiakili na kukua vizuri.   Ingawa hili linaenda kupatiwa muarubaini baada ya UTPC kwa kushirikiana na Zanzibar Presidential Delivery Bureau pamoja na Zanzibar Mult-Sectoral (ECCD) kuwapa mafunzo wanahabari kwa ufadhili wa Shirika la UNICEF Zanzibar pamoja na Big Win UK.   Ni mafunzo ya kuwajengea uwezo wa kuelimisha jamii na kuripoti habari mbali mbali zinazohusiana na ...

WAANDISHI WAPEWA SOMO HABARI JUMUISHI NA HAKI ZA WATU WENYE ULEMAVU

  NA MOZA SHAABAN, PEMBA@@@@ WAANDISHI wa habari nchi wametakiwa kujikita katika kuandika  habari  jumuishi na haki za watu wenyeulemavu, ili kuongeza upatikanaji wa haki na michango yao katika maendeleo ya taifa.  Wito huo umetolewa na Afisa Programu na Mawasiliano wa Chama cha Waandishi wa Habari wanawake Tanzania (TAMWA - Zanzibar) Khairat Ali Haji wakati wa mafunzo ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari juu ya uwandishi jumuishi.  Akizungumza katika mafunzo hayo alisema waandishi wananafasi kubwa katika kubadilisha mitazamo hasi kuhusu watu wenye ulemavu, hivyo ni vyema  kutumia nafasi walizonazo ili kuhakikisha watu wenye ulemavu wanashirikishwa katika hatua za kimaendeleo.  " Waandishi wa habari wanakua na mchango mkubwa katika kubadili mitazamo iliomo katika jamii, hivyo ni muhimu kutumia nafasi hii kubadili mitazamo hayo, kwa kuwaibua na kuwashirikisha watu wenye ulemavu katika kila hatua za kimaendeleo"alisema. Aliongeza kua, mafunzohayo ni m...

KATIBU MKUU WEMA ASISITIZA MALEZI BORA KWA WATOTO

      IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, DAR-ES-SALAAM@@@@   KATIBU Mkuu Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar Khamis Abdalla Said amesema, ili kupata taifa lenye maendeleo na wataalamu wabobevu, kila mmoja anapaswa kuekeza mapema kwa watoto.   Akifunga mafunzo ya siku nne kwa waandishi wa habari wa Zanzibar, kuhusu makuzi, malezi na maendeleo ya awali ya mtoto, alisema kuwa waandishi wanapaswa kutumia kalamu zao vizuri kuibadlisha jamii na kuwa yenye kutekeleza malezi bora kwa watoto.   Alisema kuwa, kila mmoja anapaswa kuekeza mapema kwa mtoto, hivyo ni jukumu la wanahabari kuhakikisha wazazi wanafuata utaratibu mzima wa malezi na makuzi bora ya watoto kwa kuwapatia lishe bora, afya imara, kuwapa nafasi ya kujifunza mapema na kuwa nao karibu, hali ambayo itawajenga kuwa na kipaji kikubwa ambacho kitawaleta mabadiliko chanya.   "Tusipokuwa na wataalamu tutachelewa kupata maendeleo, hivyo tuanze kumkuza mtoto katika malezi bora kuanz...

IDARA YA KATIBA NA MSAADA WA KISHERIA KUWAPA ELIMU YA KISHERIA WANANCHI WAWI LEO HII

    NANA HAJI NASSOR, PEMBA WANANCHI wa shehia ya Wawi wilaya ya Chake chake, wametakiwa kuitumia fursa ya kuhudhuria mkutano maalum wa elimu ya kisheria, ulioandaliwa na Idara ya Katiba na Msaada wa Kisheria, unaotarajiwa kufanyika asubuhi hii shehiani humo. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, Mkuu wa Divisheni ya Idara hiyo Pemba Bakari Omar Ali, alisema mkutano huo, ni maalum kwa ajili ya wananchi hao, ili kuwapa elimu na msaada wa kisheria bila ya malipo. Alisema, mkutano huo ambao utafanyika eneo la Kwa gerei Wawi, ni sehemu ya utendaji wa kazi wa kawaida wa Idara hiyo, katika kuhakikisha jamii inapata muelekeo wa kutambua haki na wajibu wao kisheria. Alieleza kuwa, zipo njia kadhaa za wananchi kujua haki zao za kisheria, moja wapo ni kuwapelekea wataalam wa sheria ndani ya shehia, na kuelezea changamoto zao. ‘’Mkutano huu ambao unatarajiwa kufanyika asubuhi hii shehia ya Wawi ni maalum, ili kuona wanapata uwelewa, lakini pia kuuliza na kutoa changamoto zao...

UTPC yawanoa waandishi wa habari Zanzibar kuhusu malezi, makuzi bora ya watoto

   NA ZUHURA JUMA, Dar-Es-Salaam@@@@ ELIMU ya malezi na makuzi bora ya watoto inahitajika katika jamii ili kuhakikisha wazazi wanalea watoto wao katika malezi yaliyobora. Akizungumza na waandishi wa habari katika Ukumbi wa wa hoteli ya Jamirex jijini Dar-Es-Salaam, Mtaalamu wa Sayansi ya Malezi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto nchini Tanzania David Gisuka alisema, kuna baadhi ya wazazi wana tabia ya kushughulikia zaidi kazi zao na kuwaacha watoto wao wapweke, hali ambayo inawasababishia udumavu wa akili na kimwili. Alisema kuwa, watoto wanahitaji ukaribu wa wazazi wao ili kujifunza mambo mbali mbali ambayo yatawajenga kiakili, hivyo ni vyema wakatenga muda maalumu kwa ajili ya watoto wao. "Mtoto anaanza kujifunza akiwa tumboni mwa mama yake, hivyo tunatakiwa kuwa karibu nao zaidi na tuwape malezi bora ili wakue vizuri, hii itamfanya awe imara na mwenye uwelewa wa hali ya juu," alisema Mtaalamu huyo. Kwa upande wake  Mkurugenzi wa taasisi ya Makuzi na Malezi Bora ya watoto Z...

WAZIRI SHATAMA AELEZEA SABABU YA MAONYESHO YA NANE 8

  NA KHAULAT SULEIMAN ,PEMBA WAZIRI wa Kilimo Mali Asili na Mifugo Zanzibar Shamata Shaame Khamis amesema Wizara imeandaa maonyesho nane nane kwa dhamira ya kuimarisha kilimo kwa dhana za kisasa pamoja na kuimarisha kilimo hai kwa manufaa ya bidha katika jamii ili kutoa fursa kwa tasisi za kiserikali na hata binafsi na wajasirimali na wananchi wote kwa ujumla. Serikali kupitia wizara ya kilimo mali asili na mifugo imekamilisha matayarisho yote ikiwa lengo ni kuhamasisha wakulima kutumia njia bunifu za kilimo cha kisasa na kuongeza uzalishaji na mbinu bora za kisasa katika kukuza pato la taifa kwa ujumla. Aliyasema hayo kwa wandishi wa habari huko katika ofisi za Wizara ya Kilimo Wete Jodari mkoa wa kaskazini Pemba wakati wa ghafla ya ufunguzi wa maonyesho ya kilimo ya nane nane ambayo yanafanyika Dole Kizimbani wilaya ya Magharibi A Unguja. Wizara ya Kilimo Mali asili na Mifugo inaendeleza mipango na mikakati iliyoanzishwa na serekali katika kuendeleza sekta ya kilimo ili kuona nch...