Skip to main content

Posts

PEMBA: WAELEZEA WALIVYOFAIDIKA NA KAMBI YA MATIBABU YA MCHO

  NA MWANDISHI WETU,@@@@ MKURUGENZI muanzilishi kutoka bilali Muslim missin of Tanzania Kairo Nbanu Alidha alisema kuwa, kwa mashirikiano ya Tigozanztel wameamua kuanzisha kambi ya matibabu ya macho siku 3 kisiwani Pemba. Alieleza kuwa tayari wamejipanga katika kuwapatia matibabu wagonjwa 1000 kwa siku, wakiwemo na waupereshi 3000 kwa siku tatu, watakazo kuwepo.  Aliyasema hayo huko katika skuli ya Uweleni wilaya ya Mkoani Mkoa wa kusini Pemba, wakati alipokuwa akitoa huduma kwa wananchi kutoka sehem mbali. Aidha aliwataka wananchi kujitokeza kwa wingi, kuja kupata huduma hiyo kwa itawasaidia wao na kuhamasisha wenzao ambao, hawakufika kwa siku hiyo. "Huduma ni bure kuanzia dawa, miwani na hata upasuwaji, kwani tunashirikiana na Wizara ya Afya, kuhakikisha wananchi wanapata huduma hiyo. Naye katibu wa CCM Neclaus Chibwana, ambaye alifika katika kambi hiyo, kwa kupata matibabu, alieleza kuwa ni vyema kwa shirika hilo, kuendelea kuja kisiwani Pemba, kwajili ya kutoa huduma hiyo,...

VIJANA WASAIDIWA VIFAA KUJIKWAMUA KIUCHUMI

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, P E MBA   KATIBU Mtendaji Baraza la Vijana Zanzibar Salum Issa Ameir amesema, wataendelea kuwaunga mkono vijana ili waweze kujiajiri na kujipatia kipato kitakachowakwamua kiuchumi.   Alisema kuwa, Baraza la Vijana limeandaa utaratibu wa kuwasaidia vijana kwa kuwapatia nyenzo muhimu za kuwawezesha kufanya kazi kwa lengo la kutengeneza ajira ili wajikwamue kiuchumi.    Alisema hayo wakati akikabidhi vifaa kwa vijana wajasiriamali ambao wamejiajiri, katika ofisi ya Wizara ya habari Gombani Chake Chake Pemba.    Alieleza kuwa, dhamira yao ni kumsaidia Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi katika kutekeleza ahadi yake kwa wananchi kuwapatia ajira laki tatu, hivyo kupitia uwezeshwaji huo wa vijana kutawasaidia kujiajiri wenyewe na kuacha kutegemea ajira Serikalini.   "Zaidi ya shilingi milioni 12,400,000 wamekabidhiwa vijana wa Wilaya zote kwa kupatiwa vifaa kwebye vikundi mbali mbali, ...

MKONO WA TEMBO WAMLAZA MWIZI CHUO CHA MAFUNZO MIEZI 6

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHAKAMA ya Wilaya Wete, imemhukumu kwenda kutumikia chuo cha mafunzo kwa kipindi cha miezi sita, Salim Suleiman Juma (29) mkaazi wa Mtambwe,   baada ya kutiwa hatiani kwa wizi wa mazao. Mshitakiwa huyo ametiwa hatiani kwa kosa la wizi wa   ndizi mkungu mmoja aina ya Mkono wa Tembo, wenye thamani ya shilingi 30,000, kwa kukisia mali ya Othman Hamad Ali . Aidha mbali na adhabu hiyo, pia mshtakiwa ametakiwa kumlipa fidia ya hilingi 30,000 muathirika wa tukio hilo, ambae ndie mkulima na mmiliki. Imeelezwa mahakamani hapo na Mwendesha mashtaka wa serikali Shaame Farhan Khamis, mbele ya Hakimu Maulid Hamad Ali, kuwa, mshitakiwa huyo alitenda kosa hilo Aprili 5, mwaka huu majira ya saa 3:30 usiku katika kijiji cha Kiapaka Mtambwe. Mshitakiwa huyo amekiri kutenda kosa hilo, baada ya kusomewa shitaka lililokuwa linamkabilia na hivyo kuamriwa aende chuo cha mafunzo miezi sita. Aidha mshitakiwa alitakiwa kulipa fidia   ya shilingi 30,000...

WAKULIMA MRADI WA VIUNGO WAKABIDHIWA VIFAA

  NA NAFDA HINDI, ZANZIBAR@@@@  WAKULIMA wanaojishughulisha na kilimo cha  mboga mboga, matunda na viungo kupitia  MRADI wa  VIUNGO (AGRI-CONNECT)  wamekabidhiwa vifaa vitakavyowasaidia kuongeza nguvu katika uzalishaji wa bidhaa bora zitakazokidhi masoko. Akizungumza katika hafla ya kukabidhi vifaa hivyo iliofanyika katika jengo la Kificho Mwanakwerekwe Meneja Mkuu wa mradi huo Simon Makobe alisema  vifaa hivyo vitatumika kusaidia kuongeza uzalishaji na kufikia malengo ya utekelezaji wa mradi huo. Alisema MRADI wa VIUNGO ulilenga mambo mbalimbali ikiwemo kufungua fursa na kuongeza mnyororo wa thamani ya mazao hapa Zanzibar pamoja na kupatiwa vifaa kwa lengo la kuwawezesha wakulima kuwa na nyenzo muhimu ili kulima kilimo bora kitakachowasaidia kujikwamua kiuchumi,”alisema.  “Ugawaji wa vifaa hivyo ni moja ya mikakati ya utekelezaji wa mradi huo pamoja na kutumia ujuzi mulioupata juu ya matumizi ya teknolojia muliyojifunza kipindi chote cha utekelez...

DK. MWINYI AFYEKA MSONGAMANO WA WANAFUNZI MWAMBE, ASHUSHA GHOROFA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ILIKUA kama ndoto, kwa siku ya kwanza kati ya zile 360 zinazounda mwaka. Ndoto hizi zilikuwa kwa waalimu, wanafunzi, wazazi, walezi wa shehia ya Mwambe Mkoani Pemba, kunawa uso mbele ya Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi. Sio tu kunawa uso, kwa maji kama ilivyozeeleka, wao walinawa kwa kumalizika skuli ya msingi ya ghorofa mbili eneo hilo la Mwambe. Hapa wazazi, walezi, wanafunzi na waalimu, maji kwenye upindo wa kucha ya mtoto mchanga, yalitosha kuwakogesha mwili mzima. Furaha yao, sio tu kuamka wakiwa wazima siku hiyo ya Januari 1, mwaka 2023, lakini ni pale waliposhuhudia jengo la kwanza la ghorofa katika eneo la Mwambe, na bahati nzuri sio la mtu binafsi, bali likiwa la serikali. WANANCHI MWAMBE Haji Omar Kheir (65), anasema aliposikia ahadi ya rais wa sasa wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, juu ya ujenzi wa skuli ya ghorofa, hakuamini. ‘’Si unajua baadhi ya wanasiasa wakitaka jambo lao, watakuahidi jambo hata ambalo yeye hajawahi...

MWAKILISHI CUP CHAMBANI YAZINDULIWA, NADHAF YATUPWA NJE

    NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ TIMU ya soka ya Nadhaf ya Wambaa, imetupwa nje kwa matuta na timu ya Mkaa, kwenye michauano ya kuwania kombe la Mwakilishi wa Jimbo la Chambani, baada ya kutoshana nguvu kwenye dakika 90. Mchezo huo uliovuta hisia za wingi, ulikuwa wa ufunguzi, ulipigwa uwanja wa Wambaa, ambapo wanacheza kwa mtindo wa mtoano, na bingwa ataondoka na kitita cha shilingi milioni 1, kutokwa kwa Mwakilishi huyo. Wakati wanaume hao wakishindwa kutambiana kwenye dakika za kawaida, hatua ya kupigiana mikaju ya penalti, ilifanyika na timu ya Nadhaf, ikipoteza mkwaju mmoja, na wenzao kundoka na yote mitano. Kabla ya ngarambe hizo, Mwakilishi wa Jimbo la Chambani Bahati Khamis Kombo, alisema huo ni mwanzo, lakini kuna mashindani makubwa zaidi ya ngazi ya shehia yanakuja. Alisema, mashindani ya msimu huu yenye zaidi ya timu 12, ni madogo na mshindi amepanga kupata shilingi milioni 1, ingawa hayanyokuja mshindi ataondoka na shilingi milioni 5. Alieleza kuwa, wame...

SHEIKH SAID, AWAONESHA NJIA WAZAZI CHUMBAGENI KUWA NA KIZAZI CHEMA

    NA SALIM HAMAD, PEMBA@@@@ WAZAZI na walezi katika shehia ya Chumbageni wilaya ya Mkoani Pemba, wamehimizwa kuwasomomesha watoto wao kitabu kitukufu cha Qu-ran, ili kupatikana kwa kizazi chenye misingi ya maadili mema leo na baadae. Shekh Said Abdalla Nasor, ametoa kauli hiyo leo Septemba 8, 2024, wakati akizungumza na wazazi, walimu na wanafunzi wa Amladrasatul Imanniya ya Chumbageni Wambaa wilayani humo, katika mahafali ya kuwatunuku vyeti wanafunzi waliomaliza juzuu 30, na tathmini ya mwaka uliopita kwa madrssa hiyo. Alisema ili kupatikana kwa viongozi bora wa nchi, maimamu, masheikhe na hata watumishi wa umma wa baadae, hakuna budi kwa wazazi katika kuwabidiisha watoto wao, kukisoma kitabu hicho. Alieleza kuwa, taifa linahitajia madaktari, wakuu wa wilaya, waalimu wa madrassa na masheikhe wenye misingi ya dhati ya dini ya kiislamu, ambapo hilo litafanikiwa, ikiwa watakisoma kwa dhati kitabu hicho. ‘’Nichukuwe nafasi hii, kuwataka wazazi na walezi wetu, kuhak...