Skip to main content

Posts

Zawadi: mwakilishi wa Konde anaepambania kuzitatua changamoto za wananchi ‘Asema, watu wayasemee mazuri anayoyatekeleza sio kumbeza’

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@   "NIMECHIMBA visima nane katika Jimbo langu, visima sita ni vipya na viwili vilikuwepo zamani lakini vilikuwa havitumiki tena kutokana na uchakavu," si maneno ya mtu mwengine bali ni ya mwakilishi wa Jimbo la Konde Zawadi Amour Nassor.   Zawadi ni mwanamke anaepambania kuzimaliza changamoto ndani ya jimbo lake ambazo zilikuwa zikimkosesha usingizi kabla ya kuwa kiongozi.   Mama huo wa makamo anaendelea kutimiza malengo yake aliyojiwekea baada ya kuingia kwenye chombo cha kutoa maamuzi, ambayo ni ndoto yake ya muda mrefu.   Katika kipindi hiki cha muda mfupi cha uongozi wake, amefanya mambo mengi ikiwa ni pamoja na uchimbaji wa visima, hali ambayo imewapunguzia usumbufu wananchi hasa wanawake na watoto ambao ndio wahanga wakubwa.   Mwakilishi huyo anasema, upatikanaji wa maji katika jimbo lake ulikuwa ni wa kusuasua kiasi ambacho watu hutumia muda mrefu kutafuta huduma hiyo na kushindwa kufanya shughuli nyengine za maendeleo. ...

WAZIRI PEMBE AISIFIA SMT KUHUSU USAWA WA JINSIA

  Waziri wa Maendeleo ya Jamii Jinsia Wazee na Watoto Mhe. Riziki Pembe Juma amesema  Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inatambua  kuwa Jinsia na Usawa ni vipengele muhimu vya kufanikisha maendeleo endelevu nchini.  Mhe. Riziki aliyasema hayo mwishoni mwa wiki wakati akifunga kongamano la vijana wanawake viongozi  kutoka nchi 16 Baraza Afrika, lililofanyika katika ukumbi wa Chuo cha Uongozi cha Mwalimi Nyerere  Kibaha,Mkoa wa Pwani.                                              Alisema masuala ya jinsia na usawa yameainishwa katika Katiba zote mbili, katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 na ya Serikali ya Mapinduzi  Zanzibar ya mwaka 1984.  Alieleza kwamba  lengo la kuainishwa humo ni katika kusimamia haki na usawa na kuhimiza ushiriki wa wanawake katika kufanya maamuzi.            ...

WADAU HAKI ZA BINAADAMU PEMBA:' UTEKELEZAJI SHERIA ZA WATU WENYE ULEMAVU BADO KITENDAWILI’

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WADAU wa haki za binaadamu kisiwani Pemba, wamegundua kuwa Zanzibar inazosheria, kanuni na sera nzuri kwa ajili ya watu wa wenye ulemavu, ingawa changamoto kubwa ni utekelezaji wake kwa vitendo. Walisema, kwa mfano ipo sheria na sera, inayotaka kila jengo la umma, liwe ni njia maalum kwa ajili ya watu wenye ulemavu, ingawa changamoto ni kutotekelezwa na mamlaka wakati wa ujenzi. Wakizungumza kwenye kikao kazi, kilichoandaliwa na Mwemvuli wa asasi za kiraia Pemba ‘PACSO’ chenye lengo la kupitisha changamoto za kisheria kwa wanawake, watu wenye ulemavu na vijana, kilichofanyika leo Disemba 16, 2023 skuli ya maandalizi Madungu Chake chake. Walisema, hata suala la ajira kwa kundi hilo, limewekwa katika sheria kama ilivyo suala la haki nyingine za kibinaadamu, ingawa shida ni utekelezaji wake. Mmoja kati ya wadau hao, Khalfan Amour Mohamed kutoka Jumuiya kwa ajili ya watu wenye ulemavu wa akili ‘ZAPDD’ Pemba, alisema inashangaaza kuona majengo y...

UCHUMI MDOGO ULIMFANYA MWANAMKE AWE KIONGOZI

  NA AMRAT KOMBO, ZANZIBAR@@@ Binaadamu siku zote hutakiwa ajuwe alipo na wapi anataka kwenda. Katika maisha hii huwa ni ndoto ambayo humpelekea mtu kupitia mengi, baadhi yao yakiwa ni mtihani mmoja baada ya mwengine. Jambo muhimu ni kutokata tamaa na kuendelea kupambana na pale unapoteleza au kuanguka unapaswa kuinuka na kuendelea na safari huku ukiwa na matumaini ya siku moja utafika huko unapokusudia kwenda. Bi Huzaima   Ali Hamdani, miaka 51, ambae ni mjasiria mali wa uchoraji piko   na biashara ya vyakula, ni mmoja wa wanawake aliyekabiliana na mithani mingi katika safari yake ya uchoraji aliyoianza 1997. Kila alipokutana na kikwazo hakukata tamaa, bali aliendelea kupambanana na   kuanza biashara nyengine, ikiwemo ya kuuza urojo, maandazi na chapati, ili kuhakikisha anajipatia kipato cha halali cha kujiendesha kimaisha. "Kila siku asubuhi nauza urojo, mandazi chapati na juisi na ikifika jioni nauza supu ya utumbo na chapati,"alisema. Alipomsikia Rais...

TAMWA yajadili na kutathmini maendeleo ya 2023 na kuunda mikakati imara ya 2024

Na Nafda Hindi, Zanzibar @@@@ Chama cha waandishi wahabari wanawake Tanzania TAMWA ZNZ, wamekutana katika mkutano wao wa kila mwaka kutathmini utekelezaji wa shughuli zake kwa mwaka unaokwisha   2023, kujadili maendeleo, changamoto pamoja na kupanga mikakati imara ya utekelezaji wa mwaka ujao 2024. Mkutano huo wa siku mbili uliofanyika katika ukumbi wa TAMWA uliowashirikisha wafanyakazi wa TAMWA ZNZ akiwemo Mwenyekiti, Wajumbe na wadau kutoka   Asasi   mbali mbali za kiraia. Mapema akifunguwa mkutano huo Mkurugenzi wa Chama cha waandishi wahabari wanawake TAMWA ZNZ Dk Mzuri Issa amesema udhalilishaji ni janga katika jamii hivyo wanaharakati wa kupinga vitendo hivyo wasichoke na waendelee kujitoa kwa lengo la kuwalinda watoto. “Udhalilishaji bado upo unaendelea hivyo wanaharakati wasichoke kupambana ili kuwasaidia watoto na wanawake kuhakikisha wanaondokana na vitendo hivyo,” Dk Mzuri Issa.   Nae Afisa mradi wa kupinga vitendo vya ukatili na udhalilishaj...

MASHEHA WAWI, WESHA WANG'AKA WANAOHARIBU NGUZO ZA MAJINA YA MITAA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MASHEHA wa shehia za Wawi na Wesha wilaya ya Chake chake Pemba, wameahidi kuwa watakula sahani moja kisheria, na mtu yeyote atakaekamatwa akihujumu nguzo zenye majina ya mitaa katika shehia hizo. Walisema, baadhi ya wananchi wamekuwa wakijaribu kuzing’oa nguzo hizo kwa maksudi, na kuwataka waache mara moja tabia hiyo, kwani atakaekamatwa, sheria itachukua mkondo wake. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi kwa nyakati tofauti, kufuatia katika baadhi ya vijiji kung’olewa nguzo hizo, walisema yeyote hatovumiliwa. Sheha wa shehia ya Wesha Haji Mohamed Ali, alisema tayari katika moja ya vijiji vyake nguzo iliyokuwa na jina la kijiji imeshang’olewa na kuwataka wananchi, wairejeshwe mara moja. Alieleza kuwa, kwa vile serikali imetumia gharama kubwa kutengeneza nguzo hizo kwa ajili ya kurahisisha shughuli mbali mbali, hatokaa kimnya hadi itakaporejeshwa. ‘’Niwaombe kama kuna mwananchi anajua taarifa za kuibiwa kwa nguzo hizo, aje anipe kwa kina,...

USHAURI WA KISHERIA WA 'CHAPO' WAZAA MAKAAZI YA KUDUMU KWA MJANE

  HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ZAKIA Rashid Baraka (36) wa Chanjamjawiri wilaya ya Chake chake, anaetgemewa na watoto sita, sasa amejengewa makaazi ya kudumu na aliyekuwa muume wake, baada ya kunufaika na ushauri wa kisheria, aliyopewa na wasaidizi wa sheri wilaya ya Chake chake. Mjane huyo, alisema baada ya kuachika na aliyekuwa muume wake na kisha kumtaka ahame ndani ya nyumba waliokuwa wamejenga pamoja kijiji cha Tundaua shehia ya Kilindi wilayani humo, alimua kufuatilia haki yake kwa wasaidizi wa sheria. Alisema, kisha mwanamme huyo alikutanishwa nae, na kutakiwa kunijenga chumba kimoja, kwa vile alishakataa kumpa chumba kimoja katika nyumba walipokuwa pamoja kindoa. Akizungumza na mwandishi wa habari hizi, nyumbani kwake Chanjamjawiri, alisema katika ujenzi wa nyumba hiyo anayoishi muume wake kwa sasa alitumia nguvu kazi na fedha taslimu zaidi ya shilingi milioni 1. Alisema kuwa, alitegemea sana baada ya kuchwa aidha engerejeshewa fedha ama kupewa haki yake ya chumba kimoj...

WAZIRI PEMBE: 'POLISI HARAKISHENI UPELELEZI KESI ZA UDHALILISHAJI'

 Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Riziki Pembe Juma amelitaka Jeshi la Polisi Zanzibar kuharakisha masuala ya upelelezi kwa kesi za vitendo vya ukatili na udhalilishaji ili kuona zinamaliza ndani ya muda mfupi. Kauli hiyo aliitoa jana katika kilele cha maadhimisho ya kufunga siku 16 za harakati za kupinga vitendo vya ukatili na udhalilishaji kwa wanawake na watoto yaliyofanyika katika kijiji cha Muyuni Wilaya ya Kusini Unguja. Mhe. Riziki alisema taarifa za Mtakwimu Mkuu wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar zinaonesha hali inatisha kwani katika kipindi cha mwezi Januari hadi Octoba 2023 jumla ya matukio 1,620 yameripotiwa ambapo matukio 1,360 yanahusu watoto, 194 wanawake na wanaume 77. Alisema pamoja na kazi kubwa inayofanywa na Jeshi la Polisi lakini bado ucheleweshwaji wa upelelezi wa matukio hayo umekuwa mkubwa hali ambayo inapelekea kesi nyingi kukaa muda mrefu katika vituo vya Polisi Zanzibar. Alisema kuendelea kwa hali hiyo itaweza kuathiri malengo ya Serik...

DC: MICHEWENI ATOA RAI ULEZI WA MAYATIMA

  NA ASHA ABDALLA , PEMBA @@@@    MKUU wa wilaya ya Micheweni Mgeni Khatibu Yahya, ame wataka wazazi na walezi, kuwa makini katika kuwalinda watoto ili waweze kuepukana na vitendo vya udhalilishaji,  ambavyo vimeshamiri nakuongezeka siku hadi siku.  Hayo aliyasema wakati alipokuwa akikabidhi misaada kwa Mayatima  kwaniaba ya Mwenyekiti wa Nuru Foundation Zainab Kombo Shaib, ambae ni Mke wa Makamo wa Kwanza wa Rais wa  zanzibar katika Mahafali ya 11 yaliyofanyika Madrassatu _ Nnisai iliopo Machomane Wilaya ya Chake Chake Mkoa wa Kusini Pemba.  Alieleza kuwa  watoto Mayatima  wanatakiwa kutunzwa vizuri na kulelewa kama Watoto wengine bila ya kubaguliwa  kwani nao wana haki ya kupata Elimu ili  waweze kufarajika katika maisha yao ya kila siku.  "Watoto Mayatima tuwapeni  Misaada kwani nawao wanahitaji upendo nafuraha ili  weweze kutimiza ndoto zao ambazo wamejiwekea kuwa viongozi wa nchi hapo baadae", alieleza....