Skip to main content

Posts

TAMWA-ZANZIBAR: 'HAILALI HADI KUWA NA SHERIA MPYA YA HABARI ZANZIBAR'

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MOJA ya sheria kongwe na inayotajwa kutokwenda sambamba na uhuru wa vyombo vya habari, ni ile nambari 5 ya mwaka 1988 ya Magazeti, Vitabu na Mawakala wa Habari Zanzibar. Ni miaka 34 sasa, sheria hii inaendelea kutumika Zanzibar, na kutajwa kuathiri na kutishia utendaji kazi wawaandishi wa habari visiwani. HISTORIA Sheria hiyo tokea mwaka 2010, ilianza harakati za kutaka kufutwa, kwa wadau wa habari kujikusanya pamoja, ili sasa iwe na sheria moya ya habari. Kwa wakati huo, tasisi za Baraza la Habari Tanzania ‘MCT’ –ofisi ya Zanzibar, vyama vya waandishi wa habari, taasisi za haki za binadamu na wizara husika, zilianza harakati hizo. Mara kadhaa, kulikuwa na taarifa kuwa, mwaka ujao au mwakani Zanzibar itapatikana sheria mpya ya habari, ambayo itakuja kufuta sheria ya Magazeti nambari 5 ya mwaka 1988 na ile ya Tume ya Utangaazji nambari 7 ya mwaka 1977. Ilikuchakua takriban miongo miwili, kupita bila Zanzibar kuwa na sheria mpya, ingawa kwa Tan...

SHERIA YA MAGAZETI ZANZIBAR 'ZIRAILI' WA UHURU WA HABARI, TAMWA- ZANZIBAR YATAKA IFUTWE

  TAMWA, Internews waungana kutaka sheria mpya ya habari Zanzibar NA HAJI NASSOR, PEMBA::- ‘’BILA ya kuathiri sheria za nchi, kila mtu yuko huru kuwa na maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, na kutafuta, kupokea na kutoa habari kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi’’. ‘’Tena pia mtu huyo ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati, na rai anayo haki ya kupewa taarifa wakati wote kuhusu matukio ya nchini na duniani kote, ambayo ni muhumi kwa maisha yake’’. Ndivyo Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, inavyoelekeza kifungu cha 18 juu ya upatikanaji na utoaji wa habari kwa raia, tena bila ya kujali mipaka ya nchi. Mwanasheria wa kujitegemea Khalfan Amour Mohamed, anasema suala la kupata habari, au kutoa ni haki ya kikatiba, ambayo inatofautiana na haki nyingine. ‘’Ukitaka kuzigawa haki hizi, basi zipo haki za kikatiba na haki nyingine zilizotengenezewa sheria yake mbali mbali, mfano haki ya elimu,’’anafafanua. Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa kuwa...

RC MATTAR: AAHIDI KUWATIMUA KAZI MASHEHA IKIWA.......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MKUU wa mkoa wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud, amewahakikishia masheha mkoani humo, kuwa watakosa kazi na kisha kusughulikiwa kisheria, ikiwa watasimama kama mashahidi kuzifanyia sulhu kesi za udhalilishaji. Alisema kwa sasa imekuwa ni mchezo endelevu mkoani humo, kwa baadhi ya masheha kujihusisha na sulhu kwa kesi za ukatili na udhalilishaji, jambo ambalo amesema sasa imetosha. Mkuu huyo mkoa aliyaeleza hayo, wakati akilighairisha kongamano la kujadili changamoto za matendo ya ukatili na udhalilishaji, lililofanyika hivi karibuni mjiji Chake chake, lililoandaliwa na Jumuiya ya Tumaini Jipya Pemba TUJIPE. Alisema kama kuna sheha ameshachoka kuhudumu kwenye nafasi hiyo, ajaribu kuzitia mkono kesi hizo, ambazo kwa sasa zimekuwa zikijotokeza siku hadi na kuvizisha juhudi za serikali na wadau wake. Alieleza kuwa, sasa kila sheha lazima ajitenge mbali na kushiriki kwenye jamvi au vikao vya sulhu, baina ya wazazi wa pande mbili, na akigundulika hatua...

TAMWA ZANZIBAR YATANGAAZA AWAMU YA PILI TUZO KWA WANDISHI WA HABARI

    CHAMA cha Waandishi wa habari TAMWA-ZNZ kimesema jitihada zaidi zinahitajika  ili kuleta mabadiliko  ya baadhi ya sheria ,sera, na mifumo iliyopo  ambayo inaonekana  bado  inamnyima fursa  mwanamke za kushika nafasi za  uongozi  ili kuhakikisha usawa wa jinsia unazingatiwa kwa kuteuliwa au kuchaguliwa  kwa upande wanafasi za kiutawala na kisiasa.   Kauli hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Chama hicho wakati alipokua akizungumza na waandishi wa habari mjini Unguja katika mkutano maalumu ulilenga kuzinduliwa kwa awamu ya pili ya tunzo za waandishi wa habari kuhusu wanawake na uongozi pamoja natakwimu. Alisema pamoja na  jitihada na hatua mbalimbali zinazochukuliwa na  Serikali  kuridhia mikataba ya kitaifa na kimataifa Pamoja na  malengo endelevu ya milenia na ASASI za kiraia zinazojihusisha na utetezi wa  haki za wanawake katika kuwajengea uwezo na kuwahamasisha kugombea nafasi mbalimbali. Alisema bado ...

MCT LAWAPA KAZI WAANDISHI WA HABARI PEMBA

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA WAANDISHI wa habari nchini wametakiwa kusoma na kuzielewa sheria zote, ili kufanya kazi ya habari kwa ufanisi na bila vikwazo. Akifungua mafunzo ya siku moja kuhusu sheria ya habari, Mkuu wa Wilaya ya Mkoani Khatib Juma Mjaja alisema,  kujua na kuzielewa sheria za habari ni muhimu sana kwa wanahabari kwani wanazitumia katika kazi zao za kila siku. Alisema kuwa, sera, kanuni, sheria na maadili ndio yanayojenga ustawi wa habari, hivyo kuna haja kwa waandishi kuwa na juhudi ya kuzisoma sheria kila siku ili kufanya kazi zao kwa ufanisi na kuepuka vikwazo. "Waandishi wa habari ni wadau wakubwa ambao wanaifanyia kazi sheria, hivyo ni lazima tuzisome na tuzijue vizuri ili kutusaidia katika kazi zetu za kihabari" alisema Mjaja. Kwa upande wake Katibu Mtendaji wa Baraza la Habari Tanzania (MCT) Kajubi Mukajanga alisema, waandishi wa habari wasipozielewa sheria, mchakato wa kupitisha sheria utakuwa kwenye mikono ya wanasheria na wanasiasa tu, hivyo wao watakuwa ...

MTOTO ALIYEDAI KUBAKWA NA DAKTARI PEMBA ASHIKILIWA POLISI

  HAJI NASSOR NA ZUHURA JUMA, PEMBA:::- JESHI la Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, linamshikilia mtoto wa miaka 16, aliyetoa taarifa ya kubakwa na daktari Is-haka Rashid Hadid, na kisha maelezo hayo, kuyakana ndani ya mahakama wa mkoa Wete. Hayo yamekuja, wakati kesi yake ikiendelea, alipotakiwa kutoa ushahidi mahakamni hapo, ingawa alipinga vikali kubakwa kwake na mtuhumiwa huyo. Mtoto huyo alitoa ushahidi mahakamani, ambao ni tofauti na na maelezo yake ya awali, aliyoyatoa kituo cha Polisi, ndipo Mwendesha Mashitaka Juma Mussa, alipotoa maelekezo ya kushikiliwa kwa mtoto huyo. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba Juma Sadi Khamis, amekiri kupokea mtoto huyo (awali aliyedai kubakwa na daktari Is-haka), kwa tuhuma za kuidanganya mahakama. ‘’Ni kweli juzi tulimpokea mtoto wa miaka 16, ambae anadaiwa kutoa ushahidi wa uongo mahakamani, na kisha kuyakana maelezo aliyoyatoa awali kituo cha Polisi,’’alisema. Ilibainika mahakamani hapo kuwa, awali hakimu aliombwa kumpeleka rumande mto...

WAZAZI WAANZA KUTOA USHAHIDI KESI YA DAKTARI PEMBA

  IMEANDIKWA NA HAJI NASSOR, PEMBA MAHAKAMA ya Mkoa Wete imeanza kusikiliza ushahidi wa kesi ya daktari Is-hak Hadid Rashid anaedaiwa kumbaka mtoto wa miaka 16. Shahidi namba moja ambae ni baba mzazi wa mtoto huyo alidai mahakamani hapo kuwa, Aprili 21 mwaka 2022 majira ya saa 10:00 jioni wakati anarudi kwenye pirika zake za kazi aliambiwa na mke wake kuwa, mtoto wao hajarudi skuli mpaka muda huo. Alidai kuwa, hakufanya wasiwasi sana kwani aliamini kuwa itakuwa yuko kwa shoga zake baadae alikwenda bondeni na aliporudi saa 11 jioni aliambiwa bado mtoto huyo hajarudi. “Nilikwenda kwa shoga zake kumuulizia, lakini hawakuwa na taarifa zozote, ndipo nikarudi nyumbani kushauriana na mke wangu na tukaamua kwenda kutoa taarifa kituo cha Polisi Madungu’, alidai baba huyo. Mama wa mtoto huyo alidai mwanawe ni mwanafunzi wa kidato cha nne, ambapo alikwenda skuli majira ya saa 4:00 asubuhi kwa vile ilikuwa ni mwezi wa Ramadhani, ingawa ilifika muda wa kurudi skuli hajafika nyumbani, ...

KESI YA DAKTARI PEMBA KUNGURUMA TENA LEO MAHAKAMANI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA:::- MAHAKAMA ya Mkoa Wete, leo Juni 15, mwaka huu inatarajia kupokea mashahidi na kuwasikiliza kwenye shauri la daktari Is-haka Rashid Hadid, wa kituo cha afya Gombani, anayedaiwa kumbaka mara tatu, mtoto wa miaka 16. Shauri hilo linatarajiwa kuendelea leo, baada wiki mbili zilizopita (Juni 1, mwaka huu) kughairishwa, kufuatia upande wa mashataka, kutopokea mashahidi wa kesi hiyo. Awali daktari huyo, alipelekwa rumade kauanzia Mei 18, mwaka huu na kutakiwa kurudi tena mahakamani hapo Juni 1, ili kuwasikiliza mashahidi. Ingawa upande wa mashataka siku hiyo, haukupokea mashahidi, na mtuhumiwa huyo kulazimika kurejeshwa tena rumande, kama sehemu ya kuupa nafasi upande wa mashtaka kuwasilisha mashahidi. Awali, Juni 1, mwaka huu mara baada ya mtuhumiwa huyo kuwasili mahakamani hapo akitokea rumande, chini ya hakimu wa mahakama maalum ya makosa ya udhalilishaji, Mwendesha mashataka Juma Mussa, aliiomba shauri hilo kughgirishwa. Alidai kuwa siku hi...