Skip to main content

Posts

ZLSC CHATAJA NAFASI YA WANASIASA UJENZI WA AMANI ZANZIBAR

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KUTOKUWA na migogoro nchini ni sababu kubwa inayopelekea kuendelea kwa shughuli za kimaendeleo na kufikia jamii yenye amani. Kauli hiyo imetolewa na Afisa Tathmini na ufuatiliaji wa mradi wa ‘Jenga Amani Yetu’,Khamis Haroun Hamad alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi juu ya nafasi ya wanasiasa kujenga amani ya Zanzibar.   Alisema, ili jamii iweze kuwa na amani na kufikia   maendeleo endelevu, kunahitaji ushirikiano wa pamoja katika kutatuwa migogoro inayoikabili jamii, huku wanasiasa wakiwa na nafasi kubwa . Alifahamisha kuwa, suala la kutatua migogoro si la mtu mmoja pekee, bali ni la watu wote, hivyo ni vyema kila mmoja kuchukuwa nafasi yake katika jamii ili lengo liweze kufikiwa. “Sisi hatuwezi kutosha lakini tukichanganyika na nyinyi mukapeleka kwa wengine, mafanikio yatapatikana kwa haraka”,alisema. Alieleza kuwa lengo la mradi huo ni kuifikia jamii na kuisambaza elimu hiyo, ili kila mmoja ahakikishe analinda haki yake ...

WANAASASI ZA KIRAIA PEMBA WAIVA UJENZI WA AMANI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA WASHIRIKI wa mafunzo juu ya namna bora ya ujenzi wa amani na kujiepusha na migogoro hasa ya kisiasa ambao ni wanaasasi za kiraia kisiwani Pemba, wamesema sasa wamepata uwelewa mkubwa wa utatuzi wa migogoro hiyo. Walisema, elimu waliopewa kupitia mradi wa ‘Jenga amani yetu Zanzibar’ unaoendeshwa na ZLSC kwa kushirikiana na tasisi ya Search for Common Ground na LHRC, imewapa mwanga mkubwa. Walisema, awali walikuwa wakizijua mbinu za kienyeji za utatuzi wa migogoro na wakati mwengine, walikuwa wakishindwa ingawa mafunzo hayo yamewajenga upya. Hayo waliyasema ukumbi wa mikutano Samail Gombani Chake chake Pemba, kwenye mafunzo yaliondaliwa na ZLSC kupitia mradi wa jenga amani yetu. Mmoja kati ya washiriki hao Abrhaman Mbarouk Juma, alisema sasa amewiva vilivyo, kuweza kuikinga au kuitatua migogoro ya kisasa itakapotokezea katika eneo lake. Nae Is-haka Sultan alisema, sasa wanaweza kuingia katika usuluhishi wa migogoro ya kisasa, kwani elimu waliopewa ...

DC: CHAKE CHAKE 'TENGENEZENI MAZINGIRA RAFIKI SASA KABLA YA UZEE'

  NA HAJI NASSOR, PEMBA JAMII nchini, imeshauriwa kutengeneza mazingira rafiki sasa ikiwemo utoaji wa huduma kwa nusu gharama, ili ndugu na jamaa zao watakapofikia umri wa uzee, iwe rahisi kuyatumia mazingira hayo, bila ya vikwazo. Ushauri huyo umetolewa na Mkuu wa wilaya ya Chake chake Abdalla Rashid Ali, alipokuwa akizungumza na wanajumuia ya Wazee na wastaafua Zanzibar ‘JUWAZA’ kwenye mkutano wa mashauriano wa utekelezaji wa haki za wazee na wastaafu, uliofanyika Chakechake. Alisema, hivi sasa kila mmoja hajaona umuhimu wa kuweka mazingira hayo rafiki na ya kudumu, kwa ajili ya wazee waliopo sasa, hadi hapo umri utakapofika na kuanza kukumbana na changamoto. Alieleza kuwa, kila mmoja na kwa nafasi yake, awe serikalini au tasisi binafsi, anapaswa kutengeneza mazingira sasa, ili akifikia uzee, apunguze vikwazo kwenye shughuli zake. “Kwa mfano hata hospitali zetu, zianze sasa kuweka madirisha maalum kwa ajili ya wazee, wenye vyombo vya usafiri waanze na nusu nauli, au kuo...

AJIRA ZA WATOTO TUMBE PEMBA SIO TISHIO LA UVUNJIFU WA AMANI

  NA HAJI NASSO,  PEMBA   ZANZIBAR ni muunganiko wa visiwa viwili Unguja na Pemba.   Kwa miaka mingi sasa visiwa hivi vimekua vikisifiwa katika suala uwepo wa amani ya kutosha visiwani humo.   Viongozi mbali mbali wa serikali, NGOs, mashirika na wadau wamaendeleo wamekua mstari wa mbele kuhimiza suala la amani na utulivu, kabla ya Uchaguzi, wakati na hata baada ya uchaguzi mkuu wa vyama vingi.   Tumekua tukizowea kuona uvunjifu wa amani hujitokeza zaidi kabla au baada ya kipindi cha uchaguzi mkuu wa vyama vingi, nakusahau muda mwengine na badala yake kutokea vurugu zinazoelekea kwenye mapigano.   Vipo viashiria vingi au sababu na maarufu vinavyopelekea uvunjifu wa amani kama vile kupindwa kwa demekrasia, kucheleweshwa kwa haki, ukosefu wa huduma za kijamii na ubaguzi.   Wengine husahau na wakati mwengine kupuuzia sababu za uwepo wa ajira za watoto kuwa zinaweza kuwa chanzo cha uvunjifu wa amani nchini.   WAZAZI...

VYAMA VYA SIASA VYATAKA MARDHIANO, AMANI ILIYOPO ZANZIBAR ISHESHIMIWE

  NA ALI SULEIMAN, PEMBA TAREHE 6 Disemaba mwaka jana, ilikuwa siku pekee ya kihistoria kwa wazanzibari kuzaliwa upya kisiasa. Hii ilikuwa ni kufuatia kitendo cha rais wa Zanzibar Dk. Hussein Mwinyi, kumteua Maalim Seif Sharif Hamad kuwa Makamu wa Kwanza wa rais . Kitendo hicho cha kikatiba, kilihusisha uungwana, ubobevu wa kisiasa, ukweli, nia ya kimaendeleo, utayari wa kuwaunganisha wazanzibari, kwa viongozi wetu hawa wawili. Maana walishasema wazee wa zamani kuwa, muungwana ni vitendo, na chanda chema huvishwa pete, haya yanashabihiana mno na hapa kwetu Zanzibar kwa tendo hilo. Maana viongozi wetu wakuu, marehemu Maalim Seif Sharif Hamad na Dk. Hussein Mwinyi ambao kwa upande mmoja ni viongozi wa vyama vya siasa, kwa kule kuungana kuunda serikali ya pamoja. Ingawa uundaji wao wa serikali hii ya Umoja wa Kitaifa, umeelezwa ndani ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kufuatia marekebisho ya 10, pia yaliofanywa mwaka 2010. Awali, Zanzibar ilishaanza mingurumo nguru...

VYOMBO VYA HABARI, DARAJA LA KUJENGA AMANI YETU ZANZIBAR VIKITUMIKA VIZURI

  NA HAJI NASSOR,   PEMBA IKUMBUKWE kuwa, mwaka 2010 na hasa baada ya marakebisho ya 10 ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, ilifuta nafasi ya Waziri Kiongozi, kuwa kama mtendaji mkuu wa serikali. Na hapo sasa, ikamtambua Makamu wa Pili wa rais kuwa ndie atakaekuwa mtendaji mkuu wa serikali, ingawa imeongeza kiongozi mwengine anaitwaye Makamu wa Kwanza wa rais. Huyu mwenyewe, hutokana na kile chama kilichoshika nafasi ya pili, kwenye chaguzi mkuu wa vyama vingi nchini, na Katiba ikimtaja kuwa atateuliwa na rais. Kumbe wa Zanzibar suala la kuwa na serikali ya Umoja wa Kitaifa sio geni, wala huu mwaka 2020 sio mara ya kwanza, maana ilianza mwaka 2010. Ingawa mwaka 2015, ilisita kidogo kwa sababu za hapa na pale, lakini mwaka huu tena, chini ya rais wa Zanzibar wa awamu ya nane Dk. Hussein Ali Mwinyi akitokea chama cha Mapinduzi ‘CCM’ imerudi tena. Na kwasasa, (marehemu) Makamu huyo wa Kwanza wa rais ni yule yule aliyeanza mwaka 2010, ingawa kwa sasa akihudumu ndani...

VIJANA PEMBA WATAKA MARIDHIANO ZANZIBAR YAENZIWE KWA VITENDO KUKINGA NA MIGOGORO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA   …..hii sio mara ya kwanza, kwa gwiji wa siasa Zanzibar Maalim Seif Sharif Hamad, kuwa Makamu wa Kwanza wa rais ndani ya serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.   Kabla ya kufutwa matokeo ya uchaguzi mkuu wa 2015, Maalim Seif, kwa wakati huo akihudumu na Chama cha Wananchi CUF, alishika nafasi hiyo kutoka 2010 hadi 2015.   Wakati huo Dk. Ali Mohammed Shein wa Chama cha Mapinduzi (CCM), akiwa Rais wa awamu ya saba, akipokea kijiti hicho kutoka kwa muasisi wa maridhiono hayo Amani Abeid Karume.   Maalim, ameamua kurudi tena kuwa Makamu wa Kwanza, kwa sasa akiwa pamoja na rais wa awamu ya nane, wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi.   Kwa ustaarabu, uvumilivu, ukongwe wa kisiasa na kuweka mbele zaidi maslahi mapana ya wazanzibari, ndio maana Disemba 8, mwaka 2020, Zanzibar ilizaliwa tena upya.   Upya wake, unakuja maana licha ya Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, kuanzia mwaka 2010 kutaka kuwepo kwa serikali ya Umaj...