Skip to main content

Posts

KAMATI YA BUNGE PIC YATEMBELEA MIRADI YA GESI ASILIA MTWARA

  NA MWANDISHI MAALUM, @@@@ Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma(PIC) imefanya ziara mkoani Mtwara na kutembelea miradi ya gesi iliyopo Msimbati na Madimba.  Akizungumza katika ziara hiyo Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi TPDC Ombeni Sefue amesema kuwa miradi hiyo ni muhimu kwa taifa ambapo asilimia 65 ya gesi hutumika kuzalishia umeme nchini.  Amesema kuwa gesi hiyo inatumika kuzalishia umeme nchini ambapo ina mchango mkubwa kwa uchumi wa nchi.   “Tumefarijika kupata fursa ya kuwaonyesha wawakilishi wa wananchi fedha za taifa hili zinavyotumika na mchango inayotolewa katika uchumi wa nchi kama mlivyosikia asilimia 65 ya umeme unaotumika nchini unatokana na gesi asili ya Songosongo na Mnazibay  tumekabidhiwa jukumu hili kubwa kwa Taifa” amesema Sefue Nae Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma Deus Clement Sangu Mbunge wa Jimbo la Kwela Zanzibar amesema kuwa ziara hiyo ni ziara maalum ya kibunge ambayo imeanzia mkoani Ta...

WAJUMBE BARAZA LA WAWAKILISHI WAJIFUNZA MAFUTA, GESI ASILIA MTWARA

   NA MWANDISHI MAALUM, @@@@ Wajumbe wa Kamati ya Bajeti ya Baraza la Wawakilishi Zanzibar Wakiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo Mwanaasha Khamis Juma wamefanya ziara mkoani Mtwara ya kutembelea miradi ya gesi asilia kwa lengo la kujifunza.    Wakiwa katika ziara hiyo ya siku Moja wametembelea visima mbalimbali ikiwemo miundombinu ya gesi  ya Mnazibay pamoja na kiwanda cha kuchakata gesi Madimba.    Akizungumza mara baada ya kuwakaribisha Mkoani Mtwara Mwakilishi wa Mkuu wa Mkoa wa Mtwara ambaye pia ni Mkuu wa Wilaya ya Mtwara Mwanahamis  Munkunda amesema kuwa gesi asilia imekuwa chachu kwa maendeleo ya mikoa ya lindi, mtwara na Tanzania kwa ujumla.   Amesema uwepo wa gesi hiyo ni fursa kubwa ambayo watajifunza na wataiona jinsi inavyofanyakazi ambapo ndio malighafi inayotumika viwandani, majumbani na pia ni nishati inayotumika kuzalishia umeme.    "Gesi kwetu ni fursa kubwa ambayo inatumika majumbaji, kwenye magari, viwandani na...

WANAWAKE TANZANIA WAWEZESHWA MANUNUZI YA UMMA KIELEKTRONIKI

    Na Salma Lusangi, New York@@@@ Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imesema imewawezesha wanawake kupata fursa za manunuzi ya umma kwa kutoa mafunzo ya kiufundi ili kuongeza uwezo wa zabuni na matumizi bora ya mifumo ya ununuzi wa kielektroniki . Taarifa hiyo imetolewa na Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia , Wazee na Watoto Mhe. Riziki Pembe Juma mwishoni mwa wiki iliyopita wakati akifunga kikao cha pembeni (side Event) huko New York, Nchini Marekani katika ukumbi wa Umoja wa Mataifa. Mhe Riziki amesema Serikali imefanya juhudi hiyo ili kuwezesha kila raia wa Tanzania kumudu faida sawa kutokana na fursa za manunuzi , hasa zile zinazohusiana na biashara ndogo ndogo zinazoendeshwa na kumilikiwa na wanawake. Amefahamisha kwamba  jitihada hiyo inafanywa na Baraza la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC), Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) na Mamlaka za Serikali za Mitaa (LGAs). Alieleza Serikali yaTanzania inasisitiza matumizi ya m...

WAZAZI WATAKIWA KUSHIRIKIANA KUDHIBITI UTORO MASOMONI

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ WAZAZI na walezi wametakiwa kushirikiana pamoja na walimu, kamati ya skuli na kamati ya shehia katika kuhakikisha wanadhibiti utoro kwa wanafunzi, jambo ambalo litasaidia kunyanyua viwango vya ufaulu. Wakizungumza na mwandishi wa habari hizi, wananchi wa shehia ya Mjiniole Wilaya ya Chajke Chake walisema, kuna baadhi ya wazazi huchangia watoto wao kuwa watoro kutokana na kuwa anapokaa nyumbani hamuulizi jambo lolote. Walisema kuwa, ushirikiano wa dhati unahitajika katika kudhibiti utoro maskulini kwa lengo la kustawisha maendeleo ya mtoto kielimu, jambo ambalo litasaidia kusoma na kufaulu vizuri kwenye mitihani yake. Mwananchi Fatma Ali Hamad mkaazi wa kijiji cha Simaongwe alisema kuwa, ni vyema kwa wazazi kuwa tayari kuwashughulikia watoto ili wapate elimu ambayo itawasaidia katika maisha yao yote. Kwa upande wake mwananchi Hamad Khatib Hamad alieleza kuwa, ingekuwa wazazi wana mashirikiano kama ilivyokuwa zamani basi suala la utoro...

BALOZI AMINA AHIMIZA WANANDOA KUSAJILI NDOA ZAO

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ MWENYEKITI wa Bodi ya Takwimu Zanzibar balozi Amina Salim Ali amewataka viongozi wa dini kuisaidia Serikali katika kuwahamasisha wanandoa kusajili ndoa, zao. Akizungumza katika mkutano wa usambazaji wa matumizi ya matokeo ya viashiria vya sensa ya watu na makaazi 2022 kwa viongozi wa dini alisema, wanandoa wengi hawana elimu ya kusajili ndoa, hivyo ipo haja kwa viongozi hao kuhakikisha wapofungisha ndoa, kuwahamasisha wanandoa kusajili ndoa zao katika mamlaka husika. Alisema kuwa, watu wengi katika jamii hawajui kwamba wanatakiwa kupata cheti cha ndoa kwa maslahi yao na Serikali kwa ajili ya kuweka takwimu sawa, hivyo viongozi wa dini wana jukumu la kuisaidia Serikali katika kutoa elimu ili wanandoa wasajili na kupata cheti. "Kwa kweli hatuna elimu hiyo kwa sababu tukipewa karatasi ya sheha au ya kutoka kwa sheikh tu basi tunatosheka na hilo, lakini kwa elimu tulioipata leo juu ya umuhimu wa cheti cha ndoa, tutakwenda kutengeneza, akinamama w...

MKAGUZI WA POLISI WETE APITA NYUMBA KWA NYUMBA KUTOA ELIMU YA MAADILI

IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ MKAGUZI wa shehia ya Mjananza Wilaya ya Wete Inspekta wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba Khalfan Ali Ussi amewataka wazazi na walezi kushirikiana katika kusimamia malezi ya watoto ili wakue katika maadili mema na kuhakikisha wanapata haki zao za msingi. Akizungumza katika muendelezo wa ziara zake ya kutoa elimu nyumba kwa nyumba kwa ajili ya kudhibiti uhalifu, Mkaguzi huyo alisema watoto wanapaswa kukua katika maadili mema hivyo ni vyema wakawasimamia ili kuhakikisha hawaharibikiwi kwenye maisha yao. Alisema kuwa, urithi pekee wa mtoto utakaomsaidia katika maisha yake ni malezi bora, elimu na afya njema, hivyo wazazi na walezi wahakikishe wanasimamia vyema kuhakikisha watoto wanapata haki zao hizo kwa ajili ya maendeleo yao ya baada Aidha aliwaomba wazazi hao kuwalinda na kuwa karibu na watoto wao ili wasifikwe na janga la udhalilishaji na ikiwa litawakuta basi wawe na moyo wa ujasiri kuwaelezea kile kinachowakuta na kuweza kuchukua hatua za...

IWEJE UVUNJIKA NDOA IWE MACHUNGU, MAUMIVU KWA WATOTO, WENGI WAELEMEWA NA MZIGO WA MTUNZO

  NA FATMA HAMAD, PEMBA …………….. SIRI ya mtungi aijuaye ni kata……… ……Wahenga wengine wakasema hasira hasara…... Misemo yote hii inasadifu mno pale ndoa inapovunjika baada ya wana ndoa kuamua lipasuke tugawane mbao. Ingawa misumari ya hizo mbao, huwachoma na kuwaumiza wengi, wakiwemo wana familia na hasa watoto wao. Mara nyingi pale wazazi wakiwa wametengana, baada ya ndoa kuvunjika watoto hukosa huduma muhimu za maisha na kuathirika kimwili na kiakili. Mwana harakati maarufu wa kulinda na kutetea haki za watoto kisiwani Pemba,Tatu Abdala Msellem, mara kwa mara amekuwa akitoa tanbihi kuwa, kuvunjika kwa ndoa isiwe sababu ya kila mzazi kufumbia macho wajibu wake wa malezi ya watoto. Hii ni kwa sababu, mtoto  anapokosa huduma za lazima sio tu huwa mnyonge na kujiona kama yatima, bali huwa hana furaha anapocheza, na akili yake huwa haifuatilii vizuri masomo. ‘’Kama ndoa imevunjika, kwanini watoto waingizwe katika shida wakati wao sio walioingia kwenye mkataba...