Skip to main content

Posts

MIKATABA YA KUWAINUA WANAWAKE IMEACHWA NYUMA

  NA ASIA MWALIM, ZANZIBAR@@@@                                        NCHI nyingi zimeridhia mikataba na matamko ya usawa wa kijinsia na uwezeshaji wanawake kwenye uongozi na nafasi za maamuzi kama ilivyoainishwa katika Tamko la Haki za Binadamu la 1948.   Zanzibar imesaini mikataba ya kikanda na kimataifa, lakini safari ya utekelezaji ni ndefu kwa sababu hadhi sawa  kwa wanawake na wanaunme katika uongozi haipo na hii inaonekana katika shehia, wadi, majimbo, wadi hata taifa kutokana na kutokuwepo fursa sawa katika kugombea uongozi.   Mara nyingi unapofanyika uteuzi nafasi wanazopewa wanawake huwa hazina hadhi sawa na zile wanazokabidhiwa wanaume na hii inapelekea wanawake kuwa na wakati mgumu kufikia malengo yao na ndio maana upo umuhimu wanawake kupaza sauti zao kutaka mabadiliko.   Vyama vya siasa navyo vinawaacha nyuma wanawake katika kuwapa nafasi za kugombe ...

WAZIRI SHAABAN ASIFIA MATUNDA YA MAPINDUZI MIAKA 60

NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WAZIRI wa Biashara na Maendeleo ya Viwanda Zanzibar Omar Said Shaaban, amesema tayari serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, imeshatekeleza mambo makubwa kwa wananchi, ikiwemo miradi mbali mbali, yenye tija ya moja kwa moja. Alisema, ndani ya shamra shamra hizi za kuelekea miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar, ni wakati kwa viongozi na wananchi kuyatangaaza mema yaliokwishafanywa, ikiwemo ujenzi wa miundo mbinu ya barabara, afya elimu na huduma za maji safi na salama. Waziri Shaaban, aliyasema hayo leo Disemba 24, 2023 kwenye hafla ya uwekaji wa jiwe la msingi la mradi wa utotoleshaji wa vifanga vya matango bahari, ikiwa ni sehemu ya shamra shamra, za kuelekea miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar, iliyofanyika shehia ya Dodo Pujini, wilaya ya Mkoani Pemba. Alisema, kwa mfano ndani ya wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi, wametafsiri kwa vitendo, maana ya Mapinduzi pamoja na yale maono ya Rais wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, la kuweka mkakati maalum katika uw...

SORAGA AWEKA JIWE LA MSINGI KITUO CHA POLISI MKOANI, AACHA UJUMBE WA MAPINDUZI

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WAZIRI wa Nchi, Ofis ya Rais, Kazi, Uchumi na Uwekezaji Zanzibar,   Mudrik Ramadhan Soroga, amesema miaka 60 ya Mapinduzi Zanzibar, imemletea heshima mzanzibari, kwa kupata haki zake bila ya ubaguzi, ikilinganishwa na kabla ya mwaka 1964. Alisema, kwa sasa kila mmoja anapata haki ya kuwasilisha lalamiko lake, katika vyombo vya sheria na kupokelewa kwa heshima na kisha kusikilizwa na uamuzi kutolewa kwa haki. Waziri Soraga, aliyasema hayo leo Disemba 22, 2023  mara baada ya uwekaji wa jiwe la msingi la kituo cha Polisi cha wilaya ya Mkoani cha daraja ‘B’ ikiwa ni sehemu za shamra shamra za miaka 60 ya Mapinduzi Zanzibar ya mwaka 1964. Alisema, sasa mzanzibari anatembea kifua mbele, akijua kuwa inapotokezea kubinywa kwa haki zake, anapopakukimbilia na kufungua mashauri, ambayo yanaendeshwa kwa haki kuanzia mwanzo hadi mwisho. Alieleza kuwa, waasisi wa taifa hili walipigania haki za wazalendo na mwendo huo unaendelezwa hadi leo ndani ya ...

Wanahabari wanawake wapewa mbinu kukwepa mitego ya udhalilishaji mitandaoni

  Na Amina Mchezo, Zanzibar@@@@ Waandishi wa habari wanawake wananafasi na mchango mkubwa katika kuielimisha jamii kupitia mitandao ya kijamii kukizingatiwa usalama wao. Akifungua mafunzo ya siku mbili  Kwa waandishi wa habar wanawake Zanzibar mkufunzi na mwanahabar mkongwe kutoka nchini Kenya  Cecilian Maundu amesema wanahabar wanawake wamekuwa wakipitia wakati mgumu wakiwasilisha kazi zao za kimtandao ukilinganisha na wanahabar wakiume. Amesema hali hiyo huwawia vigumu baadhi ya waandishi kuendelea na kazi yao na wengine kuathirika kisaikolojia kutokana na baadhi ya wafuasi wa kimtandao kuwatolea maneno ya kashfa pasi na wao kuridhia. Maundu amesema hali hiyo inaweza ikaondoka au kusaidiwa endapo kutakuwa na ushirikiano wa pamoja kati ya waandishi na taasisi za kihabar ili kuunda kikosi kazi ambacho kitamlinda mwandishi pale tu anapopata kadhia ya kimtandao. "Zanzibar mnapaswa kutumia taasisi hizi kama ZPC, TAMWA, MCT na nyengine ili pale kuona mnashambulia Kwa pamoja m...

SHAMATA AZINDUA SOKO LA KISASA MTAMBILE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ WAZIRI wa Kilimo, Umwagiliaji, Maliasili na Mifugo Zanzibar Shamata Shaame Khamis, amewaagiza wakulima wa ndizi wilaya ya Mkoani, kuepukana na vishoka wa biashara hiyo, na badala yake walitumie soko jipya la Mtambile, ili kupata bei kubwa. Waziri Shamata aliyasema hayo jana, mara baada ya ufunguzi wa soko la mboga na matunda la Mtambile wilaya ya Mkoani, ikiwa ni sehemu za shamra shamra za miaka 60 ya Mapinduzi Zanzibar ya mwaka 1964. Alisema, kuanzia sasa waachane na wanunuzi wa ndizi wanaowalalia kibei, na badala yake sasa walitumie soko hilo, ili kuzipandisha thamani ndizi zao. Alieleza kuwa, ndani ya soko hilo mtakuwa na mnada maalum wa mazao mbali mbali, ikiwemo ndizi, muhogo, matikti, nyanya, chungwa na ndimu, hivyo ni wajibu kwa wakulima hao, kulitumia soko hilo. Waziri Shamata, alisema kwa muda mrefu, wakulima walikuwa wanalaliwa kibei na wachuuzi wanaosafirisha bidhaa hiyo nje ya kisiwa cha Pemba, kwa kueleza kuwa kunaanguko la bei. ...

HIVI NDIVYO WILAYA YA CHAKE CHAKE, ILIVYOZINDUA SHAMRA SHAMRA ZA MIAKA 60 YA MAPINDUZI ZANZIBAR

  MKUU wa mko wa kusini Pemba Mattar Zahor Massoud na Mkuu wa wilaya ya Chake chake Rashid Abdalla Ali, leo waliungana na baadhi ya viongozi wa chama, serikali, vikosi vya ulinzi na usalama na wananchi wingine pamoja na wafanyakazi wa serikali, katika usafi uliofanyika barabara ya uwanja wa ndege Pemba. Ambapo zeozi hilo ni ishara ya uzinduzi wa shamra shamra za kuelekea miaka 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar, yalioasisiwa Januari 12, mwaka 1964. Kisha Mkuu huyo wa Mkoa aliwahutubia wananchi na kuwataka wayalinde mapinduzi ya Zanzibar, kwani ndio yaliowakomboa wanyonge wa taifa hili. Lakini akawakumbusha wannachi kuwa, ndani ya miaka hii 60 ya Mapinduzi ya Zanzibar, mkoa unao miradi ya maendeleo 23, ikiwemo miradi tisa ya uwekaji mawe ya msingi, miradi 10 itafunguliwa na miradi minne itazinduliwa ndani ya mkoa huo pekee. Akaeleza kuwa, zoezi la kufanya mapainduzi ya Zanzibara hapo mwaka 1964, lilikuwa gumu na zito, ingawa waasisi wa taifa hili walifanikiwa na sasa kila mmoja ameshayaona...