Skip to main content

Posts

JAJI MSTAAFU LUANDA, ACHAGULIWA RAIS MCT

    NA HAJI NASSOR, DAR-ES SALAAM@@@@ WANACHAMA wa Baraza la Habari Tanzania MCT, wamemchagua Rais mpya wa Baraza hilo, Jaji Mstaafu: Bernad Luanda, kupitia mkutano mkuu wa 26, uliofanyika Septemba 27, 2024 ofisi za ‘MCT’ Tegeta nje ya jiji la Dar-es Salaam. Kati ya wanachama hai 29, waliohudhuria mkutano huo, waliomchagua rais huyo ni wanachama 27, kura moja ikimkataa na moja iliharibika, ambapo kisha Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi Nicholaus Mwaibale alimtangaaza.   Akizungumza mara baada ya kumalizika kwa uchaguzi huo, Katib Mtendaji mpya wa baraza hilo Ernest Sungura, alisema kwa sasa baraza linakuja kivingine, lengo likiwa ni lile lile la kuwanoa waandishi wa habari. Alisema, kuanzia mwakani, MCT itakua na mradi mkubwa unaojulikana kwa jina la ‘WAJIBIKA’ ambao utakuwa wa miaka saba. Alisema, mradi huo wa paund milioni 30, utagusa karibu kila eneo, ikiwemo kuwajengea uwezo hata waandishi wa habari mmoja mmoja, kupiti vyombo vyao. Alieleza kuwa, jingi...

WAZAZI WATAKIWA KUWALEA WATOTO WAO KATIKA MAADILI MAZURI

  IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@ WAZAZI na walezi wa shehia ya Kambini Wilaya ya Wete Mkoa wa Kaskazini Pemba wametakiwa kujitathmini na kuweka mikakati katika malezi, ili jamii iwe na vijana wenye malezi bora na maadili mema. Akizungumza na wanajamii hao katika mkutano wa elimu ya udhalilishaji na kutambua haki zao, Msaidizi wa Sheria Wilaya ya Wete ambae pia ni Mkaguzi wa Shehia hiyo kutoka Jeshi la Polisi Mkoa wa Kaskazini Pemba, Khamis Shoka Ame alisema wazazi waliowengi wamefeli katika malezi. Alisema kuwa, mporomoko wa maadili wameusababisha wenyewe wazazi kwa kukosekana kwa malezi ya pamoja, hivyo kuna haja ya kujitathmini na kuweka mikakati imara ili kizazi chao kiweze kukuwa katika maadili mema na malezi bora. ‘’Watoto tunawalea sisi lakini hawaendi skuli wala madrasa, wanaingia ndani usiku mkubwa, halafu wanakwenda nae Jeshi la Polisi kusema kuwa mtoto amemshinda, lakini tujue kwamba mwenye jukumu la malezi ni wewe mzazi, hivyo tujitahidi sana kwani tunapofel...

MIAKA MINNE YA DK. MWINYI IKULU YA ZANZIBAR WAKULIMA WA MWANI SASA KUHEMEA KIVULI

                                          NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ NOVEMBA 3 ya miaka minne iliyopita, ilikuwa ndio siku ya kwanza ya Rais mpendwa wa Zanzibar Dk. Hussein Ali Mwinyi, kuwasili ndani ya Ikuklu ya Zanzibar. Kwa  wakati huo, hakuwasili akitokea nchi jirani..laaahasha alitokea kwenye viwanja alivyokula kiapo, kushika hatamu ya uongozi. Maana Dk. Mwinyi, baada ya kumalizika kwa kampeni za zaina yake, zilizotajwa kama za kisayansi, kwa kule kukutana na makundi mbali mbali, kisha wananchi walimpigia kura. Baada ya kumalizika kwa uchaguzi mkuu wa vyama vingi, Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar ZEC, ilimtangaaza Dk. Mwinyi kuwa rais wa Zanzibar kwa kupata asilimia 76.27 na kuwaacha mbali wagombea wenzake. ‘’Nimepokea ushindi kwa mikono miwili na nawashukuru wananchi wa Zanzibar, kwa kunichagua mimi na chama changu, kwa miaka mitano ijayo,’’alisema wakati huo. Kwa wananchi Za...

JAMII TOENI USHAHIDI MAHKAMANI KESI ZIPATE HATIA

  NA ZUHURA JUMA, PEMBA@@@@ WANAJAMII wametakiwa kuwa makini katika suala la kutoa ushahidi mahakamani, kwani ndio unaoweza kumtia hatiani mshitakiwa au kumuachia huru. Azungumza na wananchi wa Daya shehia ya Mtambwe Kusini, Hakimu wa Mahakama ya Wilaya Wete Maulid Hamad Ali alisema, ushahidi ni kitu muhimu katika kesi, hivyo kuna haja ya kutoa ushahidi kwa kina pale unapohitajika. Alisema kuwa, kuna makosa mbali mbali yanayotendeka katika jamii ikiwemo ya udhalilishaji, wizi na madawa ya kulevya, hivyo wasipokuwa makini katika kutoa ushahidi, washtakiwa wataendelea kuachiwa huru huku wanajamii wataendelea kulalamika. ‘’Ushahidi ndo ambao utamtia mshtakiwa hatiani au kuachiwa huru, kwa sababu unaangaliwa uzito wa ushahidi, hivyo tuwe makini tunapokwenda mahakamani kutoa ushahidi,’’ alisema Hakimu huyo. Aidha aliwataka vijana kuacha kutumia madawa ya kulevya kwani yanasababisha kujiingiza katika mambo maovu ikiwemo kuiba na hatima yake kuishia chuo cha mafunzo. Alisema kuw...

WATEULE 'EJAT' MWAKA 2023/2024 HAWA HAPA

                                 TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI Dar es Salaam, Alhamis, Septemba 19, 2024   MAJAJI saba wa Tuzo za Umahiri wa Uandishi wa Habari Tanzania (EJAT) wamehitimisha kazi ya kutathmini ubora na weledi wa kazi zipatazo 1,135 na kuwateua waandishi wa habari 72 watakaoingia katika kinyang’anyiro cha kumtambua mshindi wa kwanza, wa pili na wa tatu na mshindi wa jumla. Kati ya waandishi wa habari 72, wanaume ni 45 (sawa na 62.5%) na wanawake 27 (sawa na 37.5%). Kati ya wateule hao, wateule 14 (19%) wanatoka katika runinga; 13 (18%) wanatoka vyombo vya mtandaoni, redio 20 (28%) na wateule 25 (35%) wanatoka kwenye magazeti. Wateule wamepatikana kwa kukidhi vigezo vya ubora ambavyo ni pamoja na ukweli, usahihi, uanuai, haki, kina, utafiti, ubunifu, uvumbuzi, upekee, uchambuzi, uwajibikaji, ufichuaji maovu, uadilifu, uwasilishaji unaoeleweka na uchunguzi. Ifahamike pia kwamba vigezo ...