Skip to main content

Posts

TAMWA ZANZIBAR YAWAKARIBISHA WANACHAMA WAPYA

  Na Nafda Hindi, ZANZIBAR Mkurugenzi wa chama cha Waandishi Wahabari Wanawake Tanzania, TAMWA ZNZ Dkt Mzuri Issa amesema kujitoa na kufanya kazi kwa bidii ni nyenzo muhimu itakayosaidia kuendeleza na kuimarisha Taasisi kusonga mbele kimaendeleo. Dkt Mzuri amesema hayo wakati akifungua mkutano wa kuwatambulisha wanachama wapya waliopitishwa kwenye mkutano Mkuu wa mwaka 2024 kwa lengo la kuongeza utetezi wa haki za wanawake na watoto kupitia vyombo vya habari. Amesema Taasisi ili iweze kusonga mbele kimaendeleo inahitaji mashirikiano ya pamoja na uwajibikaji jambo ambalo linaweza kuleta mustakbali mwema kwa Taasisi, mtu mmoja mmoja na taifa kwa ujumla. “TAMWA ZNZ ilisimama kwa kujitoa sisi wanachama, tumeanzisha jengo letu jipya kwa kukatwa mishahara sisi wenyewe,” Dkt Mzuri Issa, Mkurugenzi TAMWA ZNZ. Nae Mwenyekiti wa Bodi wa Chama cha Waandishi wa habari Wanawake Tanzania, TAMWA ZNZ Asha Abdi amewahimiza wanachama hao kulipa Ada ya Uanachama kwa wakati ili kuepuka usumbufu wa kus...

BENKI YA TADB YAKABIDHI NG'OMBE 153 KWA WAFUGAJI KASKAZINI PEMBA

IMEANDIKWA NA KHAULAT SULEIMAN, SUZA   BENKI ya M aendeleo ya K ilimo Tanzania (TADB)  imekabidhi ng ’ ombe 153 wa m aziwa kwa wafugaji 153 kisiwani Pemba, ambao wameletwa ku toka Afrika Kusini.    Ng ’ ombe hao wamekabidhiwa w afugaji wa vikundi mbali mbali vya Mkoa wa Kaskazini Pemba kwa lengo la kuwa wezesha wafugaji hao kufuga kibiasha ra na ku wa leta tija.     Akikabidhi ng ’ ombe hao  Waziri wa K ilimo,  U mwagiliaji M ali a sili na Mifugo Zanzibar Shamata Shame Khamis a li i shukuru benk i hiyo kwa kushirikiana na mradi wa TI3P na Shirika la Heifer International Tanzania kwa juhudi zao za kumkwamua mfugaji wa kawaida kiuchumi na kumuwezesha k uku wa kibiashara zaidi.   Alisema kuwa, anaamini kuwa kupitia mkopo huo ng’ombe kwa wafugaji hao kutaweza kuwakwamua kiuchumi, kwani watazalisha maziwa mengi na kuuza, jambo ambalo litawapatia fedha zitakazowakwamua na maisha duni.   "Wafugaji nendeni mkafuge k...

WEPO YAWATAKA VIJANA KUJIEPUSHA NA UDHALILISHAJI, MAKUNDI MAOVU

IMEANDIKWA NA ZUHURA JUMA, PEMBA VIJANA wa kijiji cha Bwagamoyo shehia ya Piki Wilaya ya Wete Pemba wametakiwa kujiepusha na changamoto ya udhalilishaji pamoja na makundi hatarishi, ili waishi kwa amani katika jamii. Akitoa elimu kwa wananchi wa kijiji hicho, Msaidizi wa Sheria Wilaya ya Wete (WEPO) Hamad Omar Ali alisema vijana wanapaswa kujielewa na kujiepusha na mambo ambayo yataweza kuwapeleka sehemu mbaya. Alisema kuwa, ni vyema vitendo vya udhalilishaji, wizi na madawa ya kulevya vinaweza kuwasababishia wasiishi kwa amani katika maisha yao, kwani watakapokamatwa watachukuliwa hatua za kisheria, hivyo wajiepushe ili waishi kwa amani na familia zao. ‘’Vijana ni taifa la leo, hivyo mnatakiwa kufanya mambo ambayo mtaisaidia jamii yenu kupata maendeleo na sio kujiingiza katika mambo yasiyofaa, kwani mtajisababishia matatizo,’’ alisema. Alieleza kuwa, wamekuwa wakichukua juhudi mbali mbali za kuwaisaidia wanajamii kuwapa elimu ya kujua haki zao na kujiepusha na changamoto, ...

FAWE Zanzibar, UN Women zinavyowezesha Wanawake kufikia kizazi chenye Haki na Usawa Kiuchumi

KATIKA jitihada za kuhakikisha Tanzania inafanikisha utekelezaji wa malengo manne ya kizazi chenye, Jukwaa la Wanawake Wanaelimu wa Afrika, Zanzibar (FAWE Zanzibar) inawezesha wanawake Zanzibar kukabiliana na vikwazo kiuchumi. Kwa kushirikiana na UN Women Tanzania, FAWE Zanzibar inachangia ufikiaji wa malengo hayo kupitia utekelezaji wa  Mpango wa Pamoja wa Umoja wa Mataifa wa Kuharakisha Maendeleo ya Kiuchumi kwa Wanawake Vijijini (JPRWEE) unaolenga kuhakikisha ustawi wa wanawake vijijini na haki zao. Utekelezaji wa mpango huo unaenda sambamba na utoaji wa mafunzo kwa wanawake ili kuwasaidia  kupata ujuzi wa biashara, elimu ya kifedha, pamoja na fursa za kupata mikopo ili kuanzisha na kukuza biashara zao. Miongoni mwa mafanikio yaliyoelezwa na wanufaika wa mradi huo ambao unatekelezwa Mkoa wa Kusini Unguja ni kuongezeka kwa ajira, hali iliyoboresha kipato cha kaya na kupunguza utegemezi kwa waume.  Walisema mradi huo umewawezesha wanawake wengi kuanzisha biashara ndogo n...

‘CHAPO’ YAPATA MKURUGENZI MPYA

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ ALIYEKUWA Mratibu wa Jumuiya ya wasaidizi wa sheria wilaya ya Chake chake Pemba, ‘CHAPO’ Mohamed Hassan Abdalla, amechaguliwa kwa kura za ndio, kushika nafasi ya Mkurugenzi wa Jumuiya hiyo, iliyokuwa wazi. Mahamed Hassan, ambae hakuwa na mpinzani katika uchaguzi huo mdogo na wa dharura, alijizolea kura 15 kati ya kura zote 17 zizopigwa na wanachama wa CHAPO. Akitoa matokeo hayo leo Augost 31, 2024, Makamu Mwenyekiti wa kamati ya uchaguzi ya 'CHAPO' Hafidh Abdi Said, alisema wapiga kura wote, walitarajiwa wewe 23, ingawa hadi muda wa kupiga kura unafika kulikuwa na wajumbe 17 pekee. Alieleza kuwa, kwa mujibu wa katiba ya CHAPO, imeanisha idadi ya wajumbe wote, ni kufikia nusu, ili kufanya uamuzi iwe wa uchaguzi ama kupitisha ajenda. ‘’Idadi ya wanachama hai 17, kati ya 23 haijakikua katiba ya 'CHAPO' na ndio maana, tumefanya zoezi la uchaguzi na mshindi ambae ni Mohamed Hassan Aballa, kwa nafasi ya Mkurugenzi ameshinda,’’alifafanua. ...