Skip to main content

Posts

VIJANA WALIVYOPIGA HATUA KIMAENDELEO, SERIKALI YAWAPIGA MBELEKO

  NA HANIFA SALIM, PEMBA:: ‘ ’KIJANA ni mtu yeyote mwenye umri wa miaka 15 hadi miaka 35,’’ndivyo sera na sheria ya vijana Zanzibar inavyofafanua. Lakini kwa upande mwengine kijana ametafsiriwa kuwa ni mwanamke au mwanamme yeyote mwenye miaka katia ya 15 hadi 24, kama sera ya taifa ya Maendeleo na vijana ya mwaka 1996, na kama ilivyorekebishwa mwaka 2007.   K ijana ni mtu muhimu kwa taifa lolote ulimwenguni, kwani ndio nguvu kazi ya taifa, ndio taifa la kesho kama wasemavyo baadhi yao. Lakini kijana ndio tumaini la taifa na ndio mtu anayetazamiwa kwa mapana ya nchi, katika kuongoza, kukuza uchumi na kuzima majaribio ya kihalifu. Vijana wanakumbana na changamoto mbali mbali katika maisha yao, na mwisho wa siku taifa linamchukulia kama mtu aliyeshindwa na asiye na msaada wowote kwa taifa lake. Lakini katika umri huo wa ujana, inampasa kijana kujitambua ili aweze kuwa na muonekano halisi, sio kwa umri tu bali matendo zaidi. Ni lazima awe na ushawishi katika masual...

DK. MWINYI AIPA TANO MCT KIKAZI

NA MWANDISHI  MAALUM, MCT:: RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema kuwa kazi zinazofanywa na Baraza la Habari Tanzania (MCT) hususan za kutatua migogoro inayojitokeza katika sekta ya habari ni muhimu. Akizungumza na ujumbe wa bodi pamoja na watendaji wa MCT  Ikulu ya Zanzibar, Dk Mwinyi,  Desemba 22, 2022 amesema kuwa suala la maadili na weledi katika tasnia ya habari ni muhimu kusimamiwa na wanataaluma wenyewe ikiwa ni sehemu muhimu ya kukuza  na kuimarisha tasnia ya habari kwa ujumla. Amesema  kuwa kuimarisha na kuendeleza  uhuru wa habari ni muhimu kwa wadau kushirikiana kwa pamoja na kalamu za wanahabari zina  nguvu  kubwa kuliko silaha. “Kulinda uhuru wa habari ni suala la muhimu kwetu sote hivyo tushirikiane katika kulinda na kuimarisha uhuru wa habari”, alisisitiza. Akizungumzia masuala ya utafiti na majarida mbali mbali yanayochapishwa na Baraza la Habari kwa  madhumuni ya kuyatumia kukuza...

TAKWIMU ZA WAJUMBE WANAWAKE KAMATI ZA MASHEHA WANAUME WETE PEMBA ZARIDHISHA

    NA HAJI NASSOR, PEMBA:: ‘’Kamati yangu inawajumbe tisa, saba ni wanawake sawa na asilimia 77.77 na wawili ni wanaume wakiwa asilimia 22.22, na kazi zangu zinafanikiwa ,’’ndio maneno ya mwanzo ya sheha wa shehia ya Jadida Wete, Juma Ali Juma.   Awali alikuwa na kamati ya wajumbe 12, wanawake wakiwa wawili na wanaume 10, ingawa kuanzia mwaka 2020, aliivunja kamati hiyo baada ya kuona maagizo anayoyatoa, hayafanikiwi.   Mwaka 2019, alihudhuria mkutano wa ulioandaliwa na Chama cha waandishi wa habari wanawake Tanzania TAMWA- Zanzibar, Gombani Chake chake, na kuelezwa kua wanawake wana haki sawa ya kuongoza kama walivyo wanaume.   ‘’Mimi dhana hiyo niliijaribu kwenye shehia yangu, na kweli sasa wanawake ndio ninaowategemea pale ninapotoa maagizo kwa ajili ya kuwafikishia wananachi,’’anasema.   Anasema, hawajahi kushindwa kwenye shehia yake, kwa kuwa na idadi kubwa ya wajumbe wanawake, na anafikiria kuwapunguza tena idadi ya wajumbe wa...