Skip to main content

HIVI NDIVYO UISLAMU UNAVYOUKUBALI UZAZI WA MPANGO, IPO NJIA YA ENZI NA ENZELI

 



NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@

KUFUATA uzazi wa mpango, haihusiani na kuzaa watoto kidogo.

Uislamu unafafanua kuwa, hakuna uhusiano wowote kati ya kuzaa watoto kidogo, eti chanzo kikawa ni kufuata uzazi wa mpango.


Kumbe, kutajwa suala la uzazi wa mpango na Muumba, alishajua ili mtoto aweze kupata virutubisho na mjengo wa mwili, kiakili, mifupa na ngozi, anyonye maziwa ya mama yake.


Ndio maana Mhadhiri chuo Kikuu cha Zanzibar ‘SUZA’ Profesa Issa Haji Zidi, anasema uzazi wa mpango, ambao uislamu unaukubali, sio jambo kubwa, bali ni kumuacha mtoto kunyonya miaka miwili.


Kufanya hivyo, ndio hujenga huruma, mapenzi, udugu wa kiafya kuanzia ya mama na mtoto mwenye, ijapokuwa pia humpa nafasi baba kujipanga tena.


Kumbe, hata mwanamme anapata wasaa wa kucheza cheza na mke wake vyema, iwapo uzazi wao, utakuwa ni wa mpango, kama ambavyo Muumba, ameagiza.


‘’Wapo wanaume hukesha kwenye vibanda vya starehe kwa usiku mkubwa, akikumbuka kwenda kwake na idadi ya watoto wasiopishana, huona karaha,’’anasema.


Hapa Sheikh Nurdeen Kishki, anasema unaweza kuzaa watoto hadi 10 au 15, ingawa suala la uzazi wa mpango, ndio msingi mkuu.


Uislamu, unawapendelea wema mno wanandoa, na unyonyeshaji wa miaka miwili, ni kumrejeshea mama mazazi afya yake, ili kujipanga tena, kwa kushika mimba nyingine.


‘’Uislamu unavyosisitiza uzazi wa mpango, hauna jambo kubwa la kuibua mijadala, bali ni kule kutimiza haki ya mtoto, aliyezaliwa, ya kunyonya kwa miaka mwili,’’anasema.




Sheikh Salum Msabaha, akizungumza kupitia tv za kislamu za mitandaoni, anasema wala uzazi wa mpango, haujapingana na kauli ya kingozi wa waislamu, anayetaka kujifaharisha siku ya malipo, kwa kuwa na idadi kubwa ya watu.


‘’Uislamu unahimiza ya kuwa, ‘na wanawake walojifungua wanyonyeshe watoto wao miaka miwili mfululizo, ikiwa wanataka kutimiza,’’ alinukuu aya ya Qur-an.



Sheikh Abdalla Nassor Abdalla ‘Mauli’ wa Chake chake, anasisitiza kuwa, uislamu unataka watu wenye afya bora na imara, ili kuyakabili vyema mazingiara yao, ya kujitafutia chakula.


Akaenda mbali akasema, maziwa ya mama na hasa ya miaka miwili, yana virutubisho, ambavyo havipatikani kwenye nyama, samaki wala tunda la aina yoyote ulimwenguni.


Tena maziwa hayo, yanatofautiana, kati ya yale ya miezi miwili na ya baada ya kujifungu na yale ya mwaka mmoja na miezi sita, jinsi yalivyobeba virutubisho.


Kumbe maziwa ya mama, yalioingiliwa na mtoto mwengine, huzaa homoni sugu, ambazo mtoto akiyanyonya huvuruga mfumo wake wa chakula.


‘’Ndio maana, mtoto anaenyonya maziwa ya mama mwenye ujauzito, kwanza hupungua uzito, homa za mara kwa mara na baada ya wiki tatu, anaweza kutapika,’’anaeleza.

Ilishaelezwa kwenye uislamu kuwa, waumini wa dini ya kiislamu wasijiingize, wala wasiingizane kwenye madhara baina yao, ikiwemo kunyonyesha maziwa mabovu mtoto.

 

IPI NJIA NZURI YA UZAZI WA MPANGO ISIYO NA MADHARA?

Uislamu unaelewa kuwa, zipo njia kadhaa za uzazi wa mpango, ingawa unazigawa katika makundi mawili makubwa, ikiwemo zinazokubalika na zisizokubalika.


Sheikh Nurdeen Kishki, anasema njia nzuri ambayo ilikuwa ikitumiwa na hata na Masahaba, ni ile kwa mwanamme aliyekwenye ndoa, kukwepesha mbegu zake.


‘Njia ya kukwepesha, inahitaji ujasiri hasa kwa mwanamme na hasa mwenye umri wa rika la kati, ambapo njia hii, shahawa hutakiwa kutegeshewa kabla ya kuingia kwenye mji wa uzazi, ni kuzitolea nje,’’anasema.


Njia hii, inahitaji mwanamme na mwanamke jasiri, maana wapo wanaojaribu, ingawa wakati mwengine hushindwa njiani.

Sheikha Salum Msabaha, anasema njia hii haina madhara, hata chembe kwa wanandoa, na uislamu inaikubali, kwani ilishatumiwa na waliotangulia kabla.


‘’Njia ya kukwepesha bunduki (uume) ili risasi (mbegu za kiume) zisiingie ilipokusudiwa, ni nzuri ingawa mwanamke, hutakiwa kuzichuma dalili za muume wake mapema,’’anafafanua.

 

DALILI ZA MATAYARISHO YA KUKWEPESHA

Moja, inatajwa kuwa mwanamme kuongezeka joto la mwili, kuliko lile alilonalo kawaida, kwa mfano mwili huunguza mithili ya mpishi wa mikate ya bekari.


Nyingine ni kuongezeka kwa mvuto wa pumzi, kutoka nje ya tundu za pua kwenda ndani, mithili ya mtu anayefukuzwa na mnyama mkali.


Mwaname ambaye anakaribia kutoa mbegu, huanza kupoteza nguvu ghafla, na hapo mwanamke hutakiwa kumsukuma kwa mpangilio muume wake, ili kuepusha mbegu kuingia ndani ya uke.


‘’Dalili nyingine kwa mwanamme ambaye anakaribi kutaka kutoa mbegu zake za uzazi ‘sparm’ hufumba macho japo kwa sekunde tatu hadi nne, hivyo mwanamke kama yuko makini, na kuzitambua dalili hizi, anaweza kumkwepesha muume wake,’’anasema sheikh Mohamed Makame Ali.


Wanaume wamekumbushwa kuwa, nao lazima wazijue dalili ambazo, zitawaweke tayari, ili kabla ya asali ‘manii’ kutoja kwenye mji wa uzazi, waweze kukwepesha.


Moja inayotajwa, ni kujihisi kupungua uzito hasa kwenye viungo vya mwili, mithili ya kutaka kupoteza fahamu, pamoja na kupungua kasi ya awali ya kutikisika katika tendo la ndoa.


Dalili nyingine, ambayo wanawaume inawatokezea ni kumuona mwenza wake, kama anasinzia au wakati mwengine kuongeza kasi ya uvutaji pumzi tena usio wa kawaida.

 

UPI WAKATI MWAFAKA KUTUMIA NJIA YA KUKWEPESHA?

Viongozi wa dini ya kiislamu, wanashauri kuwa, wanandoa inapendeza zaidi, wafuatilie mpangilio wao wa tarehe husika, kabla ya kuingia kwenye tendo la ndoa.


Mtaalamu wa afya ya uzazi kutoka hospitali ya Chake chake Dk. Rahila Salim Omar, anasema kama wanandoa, wameamua kuifuata njia hiyo, ni vyema wakawa bega kwa bega na tarehe zao.


‘’Zipo tarehe, mwanamke baada ya kumaliza hedhi, hawezi kupata ujauzito, sasa siku hizo inashauriwa iwe ndio siku za kukutana na muume wake,’’anafafanua.




Mkufunzi wa afya ya jamii, Ali Mbarouk Omar kutoka Tume ya Ukimwi Zanzibar, anasema uzazi wa mpango kwa njia ya kukwepesha, ni moja wapo ya uhakika.


Zipo kadhaa, lakini kwenye dini ya kiislamu ambazo zimekubaliwa ikiwemo ya kukwepesha na kufuata tarehe ni nzuri na hazina madhara kiafya.

Sheikh Abdalla Nassor Abdalla ‘Mauli’ anasema kujikadiria watoto hasa kwa dhana kuwa, huna uwezo wa kuwahudumia haifai, katika uislamu.


‘’Chakufanya ni kufuata uzazi wa mpango, unaoambatana na mwanamke kunyonyesha miaka mwili mfululizo, ikiwa hakuna kikwazo cha daktari,’’anasema.


Maana wapo wanawake baada ya kuzaa, kwa kuhofia matiti yao kuanguka, hushindwa kuwanyonyesha watoto wao, jambo amblo halikubalika katika uislamu.

Uislamu unawataka watu kuoana na kuzaana kwa utaratibu na mfumo mzuri, ili kutunza na kulea maadili ya familia, kwani umeweka utaratibu wa umri wa kuzaa kati ya mtoto mmoja na mwengine (2:233).

 

WANAUME WANASEMA JUU YA NJIA YA KUKWEPESHA

Issa Othman Haji (55) mwenye watoto sita, anasema njia hiyo anaiona nzuri, ingawa kwa wanaume, wenye mke zaidi ya mmoja.

 

‘Kwa mfano nina wake wawili, sasa njia ya kukwepesha hainipi dhiki, tena ni mzuri na haina madhara, lakini sina hakika kwa wenye mke mmoja,’’anasema.

 

Adnani Ali Khamis (30) anasema yeye anatumia njia hiyo, ingawa anakwenda sambamba na kuzijua tarehe za kubeba na kutobeba ujauzito kwa mke wake.

 

Mwanamme ambae hakupenda jina lake lichapishwe, anasema njia hiyo ya kukwepesha ni nzuri, lakini inahitaji umakini mkubwa kwa wanandoa.

 


‘’Mimi mke wangu anatumia ya sindano, na hadi sasa haijamletea madhara, lakini hata hivyo mtoto wangu akiwa na mwaka mmoja na mizei sita, najaribu kukwepesha na nafanikiwa,’’anasema.

Othman Khamis Mmanga wa Chanjamjawiri, anasema mara kadhaa alijaribu njia hiyo, ingawa humshinda njiani.

 

WANAWAKE WANASEMAJE

Maryam Himid Mjaka (19) wa Wawi anasema haijaingia kwenye ndoa, lakini njia mwafaka ya kuwa na uzazi wa mpango ni kukwepesha na kutumia tarehe.

 

Aisha Mkadamu Nassor (50) wa Kengeja anasema, njia aliyokuwa akiitumia ni tarehe na kukwepesha, wakati wote wa tendo la ndoa.

 

Maimuna Ali Mohamed (22) ambae sio jina lake, anasema alijaribu kumataka muume wake akwepeshe, ingawa alishindwa na sasa anaujauzito wa miezi sita na mtoto wa mwaka mmoja.

 

‘’Baada ya kumzaa mtoto wa kwanza, nilimuuliza muume wangu, tunafanya nini, kuhakikisha namnyonyesha miaka mwili, akataka tukwepeshe, ingawa alinyonya mwaka mmoja tu,’’anafafanua.

 

TAMWA INAFANYA NINI?

Chama cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania –TAMWA Zanzibar na Tanzania bara, wanaendelea kutekeleza mradi wa majaribio wa mwaka mmoja, wa haki ya afya ya uzazi.

 


Mratibu wa mradi huo Zanzibar, Zaina Abdalla Mzee, anasema lengo ni kuwajenge uwezo waandishi wa habari, ili waweze kutoa elimu kwa wanawake, wasichana na jamii, juu ya faida za uzazi wa mpango.

 

Maradi huo, unaendeshwa katika wilaya za Magharibi ‘B’ Kati kwa Unguja na Chake chake kwa Pemba, ambapo ulikuja baada ya utafiti kugundua, elimu ya haki ya afya ya uzazi, iko chini kwa jamii.

Unatekelezwa kwa ushirikiano kati ya TAMWA-Zanzibar na wenzao wa Tanzania bara, unafadhiliwa na Shirika la Wellspring Philonthropic fund la Marekani.

Shabaha kuu ya mradi huo ni kuwajengea uwezo waandishi wahabari, ili kuripoti kwa ufanisi, juu ya haki ya afya ya uzazi kwa wanawake na wasichana walioko mjini na vijijini.

WIZARA YA AFYA

Waziri wa Afya Zanzibar Nassor Ahme Mazurui, anasema watumiaji wa njia za kisasa za uzazi wa mpango wamepungua kutoka mama 63,261 kwa kipindi cha Julai, 2020 hadi Machi, 2021 na kufikia 61,379 kwa kipindi kama cha mwaka 2021/2022.

Shirika la Afya Ulimwenguni, kwenye taafita yake ya mwaka 2022, limethibitisha kuwa matumizi ya njia za uzazi wa mpangilio, yanaweza kupunguza vifo vitokanavyo na uzazi 30, kila wajawazito 100.


                  Mwisho

 

 

 



 

 

 

 

 

 


Comments

BLOG'S VISITORS

DAKTARI MWENGINE CHAKE CHAKE KULA SIKUKUU POLISI, NI KWA TUHUMA ZA KUMBAKA MGONJWA WAKE

NA WAANDISHI WETU, PEMBA::: DAKTARI anaetoa huduma kwa wagonjwa kituo cha afya cha serikali cha  Gombani wilaya ya Chake Chake Pemba, Is-haka Rashid Hadid, anaendelea kushikiliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa kaskazini Pemba, akituhumiwa kumtorosha na kisha kumbaka mtoto wa mwenye umri wa miaka 16, mkaazi wa Gombani. Daktari huyo miaka 35 ni mkaazi wa Kangagani Wilaya ya Wete mkoani humo, ambapo anadaiwa alimchukua mtoto huyo kutoka kwa rafiki yake, na kumpeleka kwenye nyumba anayoishi eneo la Kangagani. Mtoto aliefanyiwa kitendo hicho alisema kuwa, April 21 mwaka huu alikwenda kituo cha afya Gombani, kwa ajili ya matibabu na baada ya kupatiwa huduma na daktari huyo, alimuomba nambari yake ya simu. Alisema ilipofika usiku, walikuwa wanawasiliana kupitia ujumbe mfupi (sms) kwa lengo la kwenda kuchukua dawa nyingine ambazo kwa mchana huo alizikosa hospitalini hapo. "Nilikwenda hospitali kutibiwa, baada ya kufanya mapele katika sehemu zangu za siri, lakini akaniambia mpaka aje da

'MKAPA' NA WENZAKE PEMBA WALAZWA RUMANDE

  NA HAJI NASSOR, PEMBA@@@@ MAHKAMA kuu Zanzibar kisiwani Pemba, chini ya Jaji Ibrahim Mzee Ibrahim, imewapeleka rumande watumuhimwa wanne wanaokabiliwa na tuhuma za kuua kwa makusudi, akiwemo Ali Mussa Omar ‘ Mkapa’ mkaazi wa Wawi wilaya ya Chake chake Pemba. Watuhumiwa wengine walioanza maisha mapya ya rumande ni mtuhumiwa Yassir Mohamed Juma miaka 23, Anuwari Mussa Omar miaka 30 pamoja na mtuhumiwa Yassir Mussa Omar ‘ Makababu ’ miaka 29, wote wakaazi wa shehia ya Wawi, wilaya ya Chake chake Pemba. Awali watuhumiwa hao waliwasili mahakamani hapo, kwa mara ya kwanza, kwa ajili ya kusomewa tuhma zinazowakabili za kumuua kwa maksudi Said Seif Kombo. Ilidaiwa mahakamani hapo na Mwendesha Mashtaka kutoka Ofisi ya Mkurugenzi wa Mashataka Seif Mohamed Khamis akiambatana na mwenzake Mussa Khamis Ali kuwa, watuhumiwa hao kwa pamoja wanadaia kufanya mauwaji hayo kwa maksudi. Ilidai kuwa, watuhumiwa wote kwa pamoja, walitenda kosa hilo Oktoba 16, mwaka huu, baina ya saa 7:00 mchan

HII KALI MBUNGE ASIYA AMKOGESHA MWANANCHI HADHARANI KISA HICHI HAPA......

  NA HAJI NASSOR, PEMBA MBUNGE wa viti maalum nafasi za wanawake mkoa wa kaskazini Pemba Asiya Sharif Omar, amewataka wananchi wa kijiji cha taifu, shehia ya Kinyasini jimbo la Gando wilaya ya Wete Pemba, kuyalinda miundombinu ya maji safi na salama, ili yawe endelevu kwao. Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na mwandishi wa habari hizi, mara baada ya kuwasili kijijini humo, na kumkogesha mwananchi mmoja kama ishara ya uzinduzi wa mradi wa maji safi na salama, ulioasisiwa na mbunge wa Jimbo la Gando. Alisema, hawana mbadala kwa sasa bali ni kuilinda miundombinu ya huduma hiyo, hasa baada ya mbunge wa wao Salim Mussa Omar, kuwarejeshea huduma hiyo. Alieleza kuwa, inafahamika kuwa kwa miaka 14 waliikosa huduma hiyo hasa kwa vile viongozi waliokuwepo hawakujali kuwatatulia tatizo hilo, hadi juzi ilipofanywa na mbunge wao. “Baada ya huduma hii sasa kurejeshwa na mbunge wa jimbo la Gando, kazi iliyobakia kwenu wananchi ni kila mmoja kuwa mlinzi wa miundombinu hii,’’ali

TUHMA ZA DAKTARI PEMBA KUCHIWA HURU: POLISI KASKAZINI KUTOA TAARIFA RASMI LEO

  NA HAJI NASSOR, PEMBA KAMANDA wa Polisi mkoa wa kaskazini Pemba, Juma Saad Khamis, amesema leo Mei 9, mwaka huu atatoa taarifa rasmi, juu ya kuendelea kumshikilia au kumpa dhamana ya Polisi, daktari wa Kituo cha Afya Gombani Is-haka Rashid Hadid, anayetuhumiwa kwa ubakaji. Alisema, kwa vile alikuwa katika mapumziko mafupi, haelewi jambo lolote linaloendelea kwa mtuhumiwa huyo, juu ya kuendelea kushikiliwa kwake kituoni hapo. Alieleza kuwa, leo Mei 6 (jana), hajapata taarifa za ndani za mtuhumiwa, huyo na kuwataka wananchi na wanaharakati, wasubirie hadi Jumatatu ijayo. Akizungumza na waandishi wa habari kwa nyakati tofauti Kamanda huyo, alisema hana taarifa zozote za kupewa dhamana mtuhumiwa ndani ya kituo chake cha Polisi au kuendelea kuwepo. ‘’Ilikuwa mimi sipo kazini kwa muda, kuanzia anakamatwa hadi anafikishwa Polisi, kwa sasa siwezi kueleza jambo lolote kwa mtuhumiwa huyo, hadi Jumatatu,’’alieleza. Aidha Kamanda huyo alieleza kuwa, kwa sasa hawezi kutoa ufafan

MADAKTARI KUTOKA CHINA WAOKOA MAISHA YA MTOTO PEMBA

  HABIBA ZARALI, PEMBA TIMU ya 32 ya madaktari wa kichina katika hospitali ya Abdalla Mzee Mkoani wamefanikiwa kufanya upasuaji mkubwa wa mtoto mwenye umri wa miaka 15 mkaazi wa Chole Kengeja, baada ya kuchomwa na jiti sehemu ya njia zake za mfumo wa uzazi. Mtoto huyo ambae alianguka hivi karibuni katika mti na baadae kuchomwa na jiti hilo na kumsababishia kutokwa na damu nyingi katika sehemu ya nyonga, alifanyiwa upasuaji uliodumu kwa muda wa saa tatu na   kuokolewa maisha yake. Akizungumza mara baada ya operesheni huo kiongozi wa timu hiyo Dr Jiang Jinhua, alisema mara baada ya mtoto huyo kufikishwa hospitalini hapo na kufanyiwa vipimo na kuonekana   ilibidi apatiwe rufaa ya kwenda katika hospitali nzuri yenye kutibu tatizo lake huko nchini Kuwado ambapo haikuwezekana kutokana na hali ya umaskini wa f amilia ya mtoto huyo . Alisema timu ya madaktari hao itaendelea kutowa huduma za matibabu   kwa wananchi kisiwani humo,   ili kuwaondolea gharama ya kutafuta matibabu nje ya nch